Skip to main content

Simba yaifuata Yanga Zenj

Kikosi cha Simba
WAKATI Yanga ikiwa imeondoka Dar es Salaam  kwenda Unguja na kucheza mchezo mmoja dhidi ya Mlandege ya Zanzibar na kuichapa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia leo, Simba nayo inaelekea huko leo kujiandaa kwa mchezo wao wa Ngao ya Jamii utakaopigwa Agosti 23, mwaka huu.
Yanga baada ya mchezo wao, leo imeondoka Unguja kuelekea pemba ikitakakoweka kambi yao, Simba yenyewe itaweka kambi Unguja huku ikiwa imetoka kucheza mchezo wa kirafiki jana dhidi ya Mtibwa Sugar na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam, bao lao likifungwa na Emmanuel Okwi.
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kikosi chao chote kilichosajiliwa kwa ajili ya msimu huu kitakwenda Zanzibar kwa kambi ya siku 10 kabla ya kuvaana na Yanga.
Alisema kikosi hicho kikiwa huko kinatarajwia kucheza mchezo mmoja au miwili ya  kirafiki.
Awali Simba iliweka kambi Johannesburg, Afrika Kusini kwa wiki mbili ambako ilicheza mechi mbili za kirafiki, ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Orlando Pirates kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya mabingwa wa nchi hiyo, Bidvest Wits, iliporejea nchini Ogosti katika Siku ya Simba ilishinda bao 1-0 dhidi ya Rayon Sports katika mchezo wa kirafiki.
Wakati huohuo, Uongozi wa Klabu ya Simba katika kutaka kurejeasha umoja, umesamehe wanachama 71 wa timu hiyo wa Tawi la Simba Maendeleo huku ukiwataka kufuta kesi yao waliyoifungua mahakamani.
Hatua ya kurejeshwa kwa wanachama haom ilikubaliwana na wanachama waliohudhuria  mkutanom mkuu wa klabu hiyo  uliofanyika jana Jumapili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere, Posta jijini Dar.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...