Skip to main content

Michael Jackson akumbukwa na bintiye


Paris alivyotokelezea kwenye tuzo za MTV VMA

NEW YORK, Marekani

BINTI wa aliyekuwa mfalme wa muziki wa pop duniani, Michael Jackson 'Jacko',  Paris (19) amemkumbuka baba yake  ambaye kama angekuwa hai leo angetimiza umri wa miaka 59.
Michael Jackson alizaliwa  Agosti 29,1958  na kufariki Juni 25, 2009 kwa matatizo ya shinikizo la damu.
Kwa kumkumbuka baba yake ameweka kwenye mtandao wa kijamii picha aliyopiga naye inayomwonesha akiwa binti mdogo akimbusu baba yake ambaye wakati huo alitimiza umri wa miaka 50.
Chini ya picha hiyo ameandika maneno; '' Nakutakia kheri siku ya kuzaliwa mpenzi wa maisha yangu, mtu pekee aliyenionesha mapenzi ya kweli yalivyo, mtu ambaye alinipatia ari ya kuishi na jinsi ya kupanga.


Paris (kulia) alipokuwa binti mdogo akimbusu baba yake Michael Jackson 'jacko' alipotimuza umri wa miaka 50, miaka tisa iliyopita.

“ Sitajisikia kupenda tena kama nilivyokuopenda wewe. Kila wakati uko na mimi na kila wakati nitakuwa na wewe. Ingawa mimi si wewe na wewe si mimi, ninajua kwa dhati kwamba tu wamoja. Na nafsi zetu hazitabadilika. Asante kwa muujiza, milele na kila wakati.
Wakati huohuo, binti huyo wiki hii amefanya mahopjiano na Jarida la i-D na kusema kuwa hawezi kuishi maisha ya kuingiza, anapenda kuishi aisha yake halisi akiwa kama mwanamke.
Hapendi kujinyima kula ili aonekane kuwa mwembamba, anakula baga na piza za kutosha mwanzo mwisho.
Hawezi kuvaa nguo zenye vipimo za wabunifu, kama watu wengine ana makovu na alama za michubuko, alama ya kuungua kwenye miguu na mikono yake na ana 'nyama uzembe' unaotokana na mwili kuwa na mafuta.
Anasema yeye anaishi maisha anayotaka, ni mtu na si mwanasesere. Wazo kuwa wanawake wote wanatakiwa kuwa wembamba kwa dhana ya urembo, si sahihi.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...