Skip to main content

Liverpool yapigania mashine tatu za nguvu leo

Kuanzia kushoto ni Naby Keita (amesaini na kutolewa kwa  mkopo kwa RP Leipzig ,  Alex Oxlade-Chamberlain,  Kocha  Jurgen Klopp,  Thomas Lemar  na Virgil van Dijk.

LONDON, Uingereza
LIVERPOOL itatisha msimu huu kama itafanikiwa kukamilisha usajili wa wachezaji watatu leo, siku ambayo dirisha la usajili Ulaya linafungwa.
Wachezaji ambaoinapanga kuwafungia kazi ni Alex Oxlade-Chamberlain, Virgil van Dijk na Thomas Lemar lakini Philippe Coutinho anaweza kuondola Anfield.
Leo itakuwa ni siku ya pilikapilika kwa Wekundu hao, na ina matumini usajili wake utakwenda vizuri, Kocha Jurgen Klopp anataka kuwapata wachezaji hao ili kuimarisha timu yake na kuwa ya kiushindani katika Ligi Kuu England na Ligi ya Mabingwa. 
Hadi sasa timu hiyo na Arsenal zimekubaliana kuhusu mkataba ambao ufafanya Oxlade-Chamberlain ambaye ni pia mchezaji wa timu ya taifa ya England kutua Anfield kwa ada ya pauni milioni 35, baada ya kukataa kujiunga na Chelsea iliyokuwa ikimhitaji.
Nyota huyo inadaiwa atakuwa akipata mshahara wa pauni 120,000 kwa wiki.
Liverpool imeshafanya makubaliano kuhusu maslahi binafsi na taarifa zinasema kuwa atapimwa afya St George's Park ambako anafanya mazoezi na timu ya England kabla ya mchezo wao wa kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia dhidi ya .

Pia Van Dijk anaweza kuhamia Liverpool, huku pia ikipewa nafasi ya kumnyakua kiungo wa Monaco Lemar ambaye akipatikana inaweza kumwachia Coutinho kwenda Barcelona.

Wachezaji wengine iliowasaini msimu huu ni Dominic Solanke kutoka Chelsea (bure), Mohamed Salah kutoka Roma (pauni milioni 34.3), Andy Robertson kutoka Hull (pauni milioni10) na Naby Keita ambaye imemtoa kwa mkopo kwa  timu ya RP Leipzig. 

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...