Skip to main content

Wenger awakomalia Sanchez, Ozil









LONDON, Uingereza

KOCHA mhenga Arsene Wenger wa Arsenal ni jeuri, hivyo ndivyo unavyoweza kusema.

Babu huyo aliyeinoa Arsenal kwa miaka 21, anasema yuko tayari kuwaachia wachezaji wake kama Alexis Sanchez na Mesut Ozil  kuondoka bila ya kulipwa chochote baada ya kumaliza mikataba yao, hayuko tayari kuingia mikataba mipya kwa sharti la kuongezwa mishahara mikubwa isiyolingana na uchezaji.

Kama wachezaji watatu wangeuzwa, Arsenal ingeweza kuingiza  kiasi cha pauni milioni 125 (zaidi ya sh. bilioni 366)

Mfaransa huyo ambaye timu yake ilitwaa ubingwa wa Kombe la Emirates Jumapili,  alisema hawezi kuwauza wachezaji wake waliobakiza muda mfupi na wanaotaka kuondoka kwa sababu ya  kutaka kupiga pesa tu.

Sanchez, Ozil, Alex Oxlade-Chamberlain, Santi Cazorla na Jack Wilshere ni miongoni mwa wachezaji ambao wamebakiza mwaka mmoja.

Wenger alisema msimamo wake ni kutaka kuiona wachezaji wakicheza vizuri kujituma kuonesha thamani yao na kupata mikataba mipya na si lazima kuhama.

Alipoulizwa kama anaona vizuri kwa Ozil kuondoka na kukataa mshahara wa pauni 140,000 (zaidi ya sh. milioni 410)  kwa wiki anaopata, Wenger alijibu; Ndiyo. Si suala muhimu na ninafikiri ni mfano sahihi kwa sababu kila mtu anatakiwa kucheza.

“Haiwezi kubadilika kama umebakiza miaka miwili au mmoja, unakwenda nje ya uwanja,'' alisema na kuongeza kuwa wachezaji wanatakiwa kujituma kwa kipindi chote cha mikataba yao na si kuweka masharti.

Alisema kama mchezaji ataondoka hajali. Ni kitu cha kawaida kwake na kuwashangaa waandishi ambao wanashangazwa na kitu kama hicho.

Alisema kwa baadaye waandishi wataona zaidi makocha wakikataa kuwauza wachezaji kwa kuwa ada zinakuwa kubwa sana, hakuna atataka kutoa fedha zinazotakiwa, hiyo itakuwa katika kipindi cha miaka ijayo

Taarifa zinasema mshambuliaji raia wa Chile, Sanchez atajaribu kulazimisha uhamisho wake  kwenda Manchester City katika siku za karibuni.

Sanchez alitarajiwa Arsenal juzi, lakini aliweka picha yake katika Instagram na kudai ni mgonjwa.

Kuna taarifa kuwa Sanchez anataka kujiunga na Manchester City ambayo inanolewa na Pep Guardiola.

Arsenal  ina wachezaji nane ambao wamebakiza mwaka mmoja kwenye mikataba yao .

Ciao....

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...