NYON, Uswisi
TIMU za Afrika Kusini na Senegal zitarudiana tena baada kucheza mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 Novemba 2016 na matokeo yake kufutwa huku hukumu ya kufungiwa maisha ya refa raia wa Ghana
![]() |
Joseph Lamptey (kushoto). |
Katika mchezo wa awali uliopigwa Novemba 12 mwaka jana Afrika Kusini ilishinda mabao 2-1, lakini Lamptey aliadhibiwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (Fifa) kutojihusisha na mpira wa miguu maisha yote kwa upangaji matokeo.
Adhabu ya kufungiwa kwa Lamptey imekaziwa na CAS jana Jumatano, kwa hiyo sasa Afrika Kusini na Senegal zitarudiana Novemba mwaka huu.
''Kamati ya Fifa inayoratibu michezo ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia imeamuru kurudiwa kwa mchezo kati ya Afrika Kusini na Senegal uliofanyika Novemba 12, 2016,'' inasomeka sehemu ya taarifa ya Fifa.
''Uamuzi huu unafuatia kuthibitishwa na Mahakama ya Usuluhisi wa Michezo (CAS) kukazia hukumu ya refa, Joseph Lamptey kufungiwa maisha kwa upangaji matokeo, uamuzi uliotolewa na Kamati ya Nidhamu ya Fifa na Kamati ya Rufaa.
'' Mechi hiyo itachezwa ndani ya Novemba 2017 katika kalenda ya kimataifa, tarehe maalumu itathibitishwa.''
Afrika Kusini ni ya mwisho katika Kundi D ikiwa na pointi moja baada ya kufutwa kwa matokeo ya mchezo kati yake na Senegal ambalo Burkina Faso inaongoza ikiwa na pointi 6 sawa na Cape Verde iliyo katika nafasi ya pili zikitofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, Senegal ni ya tatu ikiwa na pointi 5.
Comments
Post a Comment