Skip to main content

Simba yapania kumburuta mahakamani Buswita

 Pius Buswita
KLABU ya Simba imesema itampeleka mahakamani,  kiungo Pius Buswita baada ya kufanya udanganyifu kwa kusaini mkataba wa kujiunga na klabu yao kisha kusaini mkataba mwingine na Yanga.
Awali Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilitangaza kumfungia mchezaji huyo mwaka mmoja kwa kusaini mkataba wa kujiunga na klabu mbili tofauti.
 Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema leo wanakusudia kumpeleka mahakamani Buswita kwa kusaini mkataba wa kujiunga nao, kisha akasaini mkataba mwingine na timu nyingine (Yanga).
"Tulikosa mawasiliano na mchezaji huyo mara baada ya kuingia naye mkataba jambo ambalo lilisababisha tushindwe kupeleka jina lake TFF kutokana na kushindwa kukamilisha baadhi ya taratibu," alisema.
Amesema watampeleka mahakamani kwa kuwa walimpatia fedha na hajarudisha, alisaini mktaba mbele ya mashahidi.
Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa akizungumzia suala hilo amesema anashangazwa na uamuzi uliochukuliwa na TFF kumfungia Buswita wakati Yanga imekamilisha taratibu zote, ikiwemo kuliingiza jina lake katika usajili wa mtandao na klabu yake kutoa ruhusa ya kumwachia kwao.
Mkwasa amesema anashangaa  TFF hawaihoji Simba kwa kuingia kwa kuwa na mkataba unaoonesha kusainiwa  Juni 2, mwaka huu kipindi ambacho mchezaji huyo alikuwa bado na mkataba na Mbao FC, kitu ambacho kinatoa nafasi kwa Mbao kuishitaki Simba.

Comments

Popular posts from this blog

Mbappe apewa jezi Na 29 PSG, acheka na Neymar mazoeni

Kylian Mbappe kushoto akisalimiana na  Neymar PARIS, Ufaransa MSHAMBULIAJI kinda Kylian Mbappe (18) baada ya kuhamia katika timu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Monaco ametambulishwa na amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na mchezaji ghari zaidi duniani,Neymar Santos . Kylian Mbappe akiwa ameshika jezi namba 29 wakati wa kutambulishwa rasmi  jana.(wapili kulia) ni baba yake, Wilfried kaka yake Ethan (watatu kulia na wanafamilia wengine. Neymar anachezea pia timu ya Brazil amesajiliwa na PSG kwa  kwa pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 578) na kuweka rekodi mpya ya usajili duniani akitokea Barcelona, ikiwa ni kiasi kilichoandikwa katika mkataba wake kinachoitaka timu inayomtaka kulipa kiasi hicho. Mbappe katika mkataba wake mpya na PSG kuna kipengele kuwa na chaguo la kuingia mkataba wa kudumu kwa ada ya pauni milioni 166 (zaidi ya sh. bilioni 484) Julai mwakani. Kama atasainiwa kwa kiasi hicho yeye na na Neymar pe...

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...