Skip to main content

Martin wa Yanga avalishwa viatu vya Msuva Taifa Stars




Emmanuel Martin  (kushoto)  akishangilia  pamoja na  Obrey Chirwa aliyembeba Simon Msuva baada ya kuifungia Yanga bao katika moja ya mechi za Ligi Kuu msimu uliopita kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mwandishi wetu
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Emmanuel Martin amevalishwa viatu vya Simon Msuva katika timu ya taifa, Taifa Stars iliyokusanyika kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa  dhidi ya Botswana Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga amemchukua mshambuliaji huyo kwa kuwa ameonesha kiwango kizuri katika mechi mbili za mwanzoni mwa msimu huu ambapo Yanga ilicheza na Simba mkicha Lipuli FC katika Ligi Kuu na michezo ya kirafiki.
Kama alivyo Msuva, Martin amekuwa akicheza kwa kujituma wakati mwingine akirudi hadi nyuma kusaidia ulinzi kucheza kati katika pamoja na wingi ya kulia na kushoto.
Mayanga, amechukua uamuzi wa kumwita nyota huyo baada kuna uwezekano akawakosa Msuva anayecheza soka la kulipwa timu ya Difaa El Jadidah ya Morocco na Orgenes Mollel wa FC Famalicao ya Ureno, kutokana na taratibu za kupata viza zimekuwa na mlolongo
Martin alijiunga na kambi ya Taifa Stars jana na kuanza na mazoezi na wenzake kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Wachezaji wa kimataifa wengine wa tanzania wanaocheza soka nje walioripoti ni Mbwana Samatta (KRC Genk/Ubelgiji), Elias Maguli (Dhofar FC/Oman), Abdi Banda (Baroka FC/Afrika Kusini), Hamis Abdallah (Sony Sugar/Kenya) wakati Farid Mussa wa CD Tenerif ya Hispania alitarajiwa kutua jana.
Wachezaji walioitwa kwenye timu hiyo ni makipa, Aishi Manula (Simba SC), Mwadini Ally (Azam FC) na Ramadhani Kabwili (Yanga).
Walinzi ni Gadiel Michael (Yanga), Boniface Maganga (Mbao FC), Kelvin Yondani (Yanga), Salim Mbonde (Simba SC) na Erasto Nyoni (Simba SC).
Viungo ni Himid Mao (Azam FC), Mzamiru Yassin (Simba SC), Said Ndemla (Simba SC), Shiza Kichuya (Simba SC) na washambuliaji ni Raphael Daud (Yanga) na Kelvin Sabato (Azam FC).
Katika benchi la ufundi pamoja na Kocha Mayanga  wengine ni, Fulgence Novatus (Kocha Msaidizi), Patrick Mwangata (Kocha wa Makipa), Danny Msangi (Meneja), Dkt. Richard Yomba (Daktari wa timu), Dkt. Gilbert Kigadye (Daktari wa Viungo) na Ally Ruvu (Mtunza Vifaa).

Comments

Popular posts from this blog

Mbappe apewa jezi Na 29 PSG, acheka na Neymar mazoeni

Kylian Mbappe kushoto akisalimiana na  Neymar PARIS, Ufaransa MSHAMBULIAJI kinda Kylian Mbappe (18) baada ya kuhamia katika timu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Monaco ametambulishwa na amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na mchezaji ghari zaidi duniani,Neymar Santos . Kylian Mbappe akiwa ameshika jezi namba 29 wakati wa kutambulishwa rasmi  jana.(wapili kulia) ni baba yake, Wilfried kaka yake Ethan (watatu kulia na wanafamilia wengine. Neymar anachezea pia timu ya Brazil amesajiliwa na PSG kwa  kwa pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 578) na kuweka rekodi mpya ya usajili duniani akitokea Barcelona, ikiwa ni kiasi kilichoandikwa katika mkataba wake kinachoitaka timu inayomtaka kulipa kiasi hicho. Mbappe katika mkataba wake mpya na PSG kuna kipengele kuwa na chaguo la kuingia mkataba wa kudumu kwa ada ya pauni milioni 166 (zaidi ya sh. bilioni 484) Julai mwakani. Kama atasainiwa kwa kiasi hicho yeye na na Neymar pe...

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...