Skip to main content

Manula aongeza utamu Simba Sauzi










KAMBI ya timu ya Simba  iliyopo nchini Afrika Kusini katika mji wa  Eden Vale, Johannesburg itachanganya zaidi kutokana na mlinda mlango Aishi Manula kuungana na wachezaji wenzie baada ya uongozi Msimbazi kumalizana na klabu ya Azam aliyokuwa akiichezea, ambayo amebakiza siku chache za kukamilisha mkataba wake.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa leo. Manula atatua bondeni kesho na kuanza kujifua na wenzie kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu 2017-18 Kombe la Shirikisho na mashindano mengine.

Manula anajiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kuichezea Azam kwa zaidi ya misimu mitano akitokea katika akademi ya klabu hiyo.

Hapa ni taarifa rasmi ya Simba iliyotolewa na Ofisa Habari wake, Haji Manara.




SIMBA SPORTS CLUB
DAR ES SALAAM
31-7-2017

         
            TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
__________________


Golikipa wa kimataifa wa Tanzania Aishi Salum Manula kesho tarehe moja,anatarajiwa kujiunga rasimi na kambi ya klabu yetu ya Simba iliopo Eden Vale Johannesburg, nchini Afrika kusini.

Manula ambae ndio Golikipa namba moja wa nchi hii ameshamalizana kila kitu kuhusu kujiunga na klabu yetu,na ameahidi kuwapa furaha wanachama na washabiki wetu,sambamba na kuisaidia klabu kushinda mataji itakayowania msimu huu.

Wakati huo huo kesho timu ya Simba inatarajiwa kucheza mechi ya kwanza ya maandalizi ya msimu dhidi ya mabingwa wa zamani wa Afrika Orlando Pirates ya nchini Afrika kusini.

Orlando ambayo ndio klabu maarufu zaid nchini humo,imeahidi kushusha silaha zake zote muhimu ili kuwapa maandalizi ya kutosha Simba,Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwenye dimba la Orlando liliopo jijini Johannesburg.

Mechi nyingine ya mwisho itakayochezwa na Simba nchini humo itapigwa siku ya Alhamis ya wiki hii dhidi ya mabingwa wa soka nchini humo kwa sasa Bidvest

IMETOLEWA NA...

HAJI MANARA

MKUU WA HABARI WA SIMBA

SIMBA NGUVU MOJA

Comments

Popular posts from this blog

Mbappe apewa jezi Na 29 PSG, acheka na Neymar mazoeni

Kylian Mbappe kushoto akisalimiana na  Neymar PARIS, Ufaransa MSHAMBULIAJI kinda Kylian Mbappe (18) baada ya kuhamia katika timu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Monaco ametambulishwa na amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na mchezaji ghari zaidi duniani,Neymar Santos . Kylian Mbappe akiwa ameshika jezi namba 29 wakati wa kutambulishwa rasmi  jana.(wapili kulia) ni baba yake, Wilfried kaka yake Ethan (watatu kulia na wanafamilia wengine. Neymar anachezea pia timu ya Brazil amesajiliwa na PSG kwa  kwa pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 578) na kuweka rekodi mpya ya usajili duniani akitokea Barcelona, ikiwa ni kiasi kilichoandikwa katika mkataba wake kinachoitaka timu inayomtaka kulipa kiasi hicho. Mbappe katika mkataba wake mpya na PSG kuna kipengele kuwa na chaguo la kuingia mkataba wa kudumu kwa ada ya pauni milioni 166 (zaidi ya sh. bilioni 484) Julai mwakani. Kama atasainiwa kwa kiasi hicho yeye na na Neymar pe...

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...