Skip to main content

Kuwaona Mayweather, McGregor laki 290








Kuwaona Mayweather, McGregor laki 290

NEW YORK, Marekani

EDDIE Hearn amesema bondia Floyd Mayweather anataka mashabiki wa Uingereza kulipa pauni 100 (zaidi ya sh. 290,000) kwa kila mtu ili kuona katika televisheni pambano lake dhidi ya Conor McGregor, lakini kituo cha Sky kinataka iwe pauni 19 (zaidi ya sh. 55,000).

Huku zikiwa zimesalia wiki nne, mashabiki bado hawajatangaziwa rasmi kuhusu ni kiasi gani watalipia ili kuona moja kwa moja pambano hilo kwenye runinga na ni kituo gani kitarusha.

Eddie Hearn ambaye ni kocha wa masumbwi, amesema anahisi Mayweather atachaji kiasi hicho cha fedha kwa pambano lao litakalofanyika Agosti 26, mwaka huu mjini Las Vegas.

Wakati wa pambano kati ya Mayweather  dhidi ya Manny Pacquiao mwaka 2015, kiasi cha juu cha kuona pambano hilo ilikuwa ni dola 89.99 (zaidi ya sh.200,000  na  dola 99.99 (zaidi ya sh 220,000.

Katika mahojiano kati ya Eddie Hearn na GQ alisema Mayweather anapenda kiasi cha kuonesha pambano hilo katika runinga kuwa pauni 100, Uingereza kiwango ambacho kama kitatangazwa kitakuwa kikubwa zaidi, cha kawaida ni wastani wa pauni 15 (zaidi ya sh.40,000).

Wakati  huohuo, mauzo ya tiketi za mchezo huo yameendelea kusuasua kutokana na kinachooonekana kiingilio chake kuwa kikubwa.

Hadi kufikia Jumamosi mamia kwa maelfu ya viti vya uwanja wa T-Mobile vilikuwa bado havijapata watu kutokana na tiketi zake kutonunuliwa.

Bei ya tiketi  inafika hadi pauni 2,665 (ambazo ni zaidi ya sh. milioni 7 za Tanzania), inawezekana mashabiki wanasubiri kama inaweza kupungua.

Hata hivyo promota Leonard Ellerbe haonekani  kuwa na wasiwasi anasema anatumini zitanunuliwa na mapato yake kuvunja rekodi.

Mapato katika pambano kati ya Mayweather dhidi ya Pacquiao mwaka  2015 yalikuwa pauni 54,974,873  (zaidi ya sh. bilioni 161) ikiwa ni makubwa mara tatu zaidi ya mapato makubwa yaliyowahi kutokea.

Viti vya karibu na ulingo kiingilio chake ni pauni 7,600  (zaidi ya milioni 22) huku tiketi viti vingine vya karibu zaidi vikilipiwa kwa pauni 11,417 (zaidi ya sh. milioni 33)

Comments

Popular posts from this blog

Mbappe apewa jezi Na 29 PSG, acheka na Neymar mazoeni

Kylian Mbappe kushoto akisalimiana na  Neymar PARIS, Ufaransa MSHAMBULIAJI kinda Kylian Mbappe (18) baada ya kuhamia katika timu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Monaco ametambulishwa na amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na mchezaji ghari zaidi duniani,Neymar Santos . Kylian Mbappe akiwa ameshika jezi namba 29 wakati wa kutambulishwa rasmi  jana.(wapili kulia) ni baba yake, Wilfried kaka yake Ethan (watatu kulia na wanafamilia wengine. Neymar anachezea pia timu ya Brazil amesajiliwa na PSG kwa  kwa pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 578) na kuweka rekodi mpya ya usajili duniani akitokea Barcelona, ikiwa ni kiasi kilichoandikwa katika mkataba wake kinachoitaka timu inayomtaka kulipa kiasi hicho. Mbappe katika mkataba wake mpya na PSG kuna kipengele kuwa na chaguo la kuingia mkataba wa kudumu kwa ada ya pauni milioni 166 (zaidi ya sh. bilioni 484) Julai mwakani. Kama atasainiwa kwa kiasi hicho yeye na na Neymar pe...

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...