![]() |
| Mashabiki wa Yanga |
KLABU ya Yanga imeungana na Simba kwa kudhaminiwa na Azam TV ambayo itakuwa ikirusha mambo yake ya michezo na maendeleo baada ya kuingia mkataba wa miaka mitatu na Kampuni ya Uhai Production Media Group.
Kwa kuingia mkataba huo juzi, matangazo Yanga sasa yataanza kurushwa katika kipindi cha television kitakachojulikana kama ‘Yanga TV’ katika moja ya chaneli za Azam TV.
Simba ilishaingia mkataba huo muda mrefu na vipindi vyake kurushwa kipindi chake katika Simba TV.
![]() |
| Moja ya magari ya Azam TV yenye mitambo ya kusaidia kurusha moja kwa moja matangazo. |
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga, amekiri kusaini mkataba wa miaka mitatu na Azam TV ambapo mbalia ya kupata kipato, sasa matukio mbalimbali ya klabu hiyo yatarushwa na mashabiki kuona kwenye televisheni.
“Ni kweli tumesaini mkataba wa kurusha matangazo yetu Azam TV, ingawa siyo suala geni sana kwetu kwani huko mwanzo tuliwahi kufanya nao mazungumzo kabla hata ya Simba ambao wao waliingia nao makubaliano kipindi hicho.
Alisema klabu hiyo imekubali kuingia mkataba na Azam Tv kwa lengo la kufungua vyanzo vingi vya mapato yatakayosaidia kuendesha gharama za Klabu
Sanga anakaimu nafasi ya uenyekiti baada ya Yusuf Manji kujiuzulu kwa sababu za kiafya.


Comments
Post a Comment