Mwandishi wetu
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa ratiba mpya ya Ligi Kuu baada ya wajumbe waliochaguliwa kufanya mapitio katika ratiba ya awali na kufanya marekebisho kama wakibaini upungufu kukamilisha kazi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya iliyotolewa na Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Alred Lucas, mabingwa watetezi Yanga watapambana na watani wao wa jadi Simba Oktoba 28, mwaka huu katika mzunguko wa nane huku mchezo wa marudiano ukipangwa katika mzunguko wa 23, Machi 14 mwakani, lakini itategemea ushiriki wao katika Mashindano ya Kimataifa ya Klabu bingwa na Shirikisho.
Tofauti na kipindi cha nyuma ambapo timu ya Azam ilikuwa ikicheza mechi zake za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, safari hii itatumia uwanja wake wa Azam Complex ambao una uwezo wa kuchukua mashabiki 7,000.
Ratiba mpya, imezingatia kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (Fifa) na ile ya Shirikisho la Afrika, baada ya michezo ya Agosti 26 na 27, Ligi Kuu ya Vodacom kwa sasa itaendelea Septemba 9 na 10 mwaka huu.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Yanga, baada ya kucheza na Lipuli na kutoka nayo sare ya bao 1-1 na Lipuli, Jumamosi ijayo itacheza dhidi ya Njombe Mji, kisha kwenda kucheza na Majimaji, Songea, kabla ya kurejea Dar es salaam kucheza na Ndanda katika mchezo wa mzunguko wa nne Septemba 23 , mwaka huu.
Simba iliyoanza ligi kwa ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting itacheza ugenini dhidi ya Azam Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Azam Complex, kisha kucheza na Nyumbani Uwanja wa Uhuru dhidi ya mwadui katika mzunguko wa tatu kicha kwenda kucheza na Mbao FC katika mzunguko wa nne Septemba 21 na kuchuana na Stand United katika Uwanja wa Kambarage Oktoba Mosi, mwaka huu.
Mechi za mwisho katika ligi hiyo zitafanyika Mei 26 mwaka huu.
Ifuatayo ni ratiba kamili ya Ligi Kuu ya Vodacom.







Comments
Post a Comment