Skip to main content

West Ham yaonja ushindi England, msimamo ulivyo kwa sasa

Andre Ayew akishangilia baada ya kuifungia West Ham bao la pili katika mchezo Ligi Kuu England dhidi ya Huddersfield  usiku wa kuamkia leo kwenye Uwanja wa London, Uingereza. West Ham United ilishinda mabao 2-0.
LONDON, Uingereza
TIMU ya West Ham imepata ushindi wake wa kwanza katika Ligi Kuu England baada ya kuichapa timu iliyopanda faraja msimu huu Huddersfield mabao 2-0.
Kipigo hicho pia kimekuwa cha kwanza kwa Huddersfield ambayo iko nafasi ya sita kwenye msimamo ikiwa na pointi saba, ambayo katika mechi zake tatu zilizotangulia, ilishinda mbili kutoka sare moja.
Matokeo hayo yameifanya, West Ham kupata pointi tatu za kwanza baada ya kupoteza mechi tatu za kwanza, iko katika nafasi ya 18 kwenye msimamo wa timu 20.
Mabao ya ushindi ya West Ham, inayonolewa na Kocha Slaven Bilic yalifungwa na Pedro Obiang dakika ya 72 ambaye alipiga shuti lililombabatiza mgongoni Mathias Jorgensen na kumpita mlinda mlango Jonas Lossl.
Javier Hernandez alipiga shuti na kugonga mwamba na kufanya West Ham kupoteza nafasi nyingine ya kufunga.
Andre Ayew aliyetokea benchi alifunga bao la pili West Ham dakika tano baadaye.
Huku zikiwa zimesalia  dakika 10, mshambuliaji wa Huddersfield, Thomas Ince alipiga mpira na kugonga mwamba.
Ufuatao ni msimamo wa Ligi Kuu England baada ya kuisha mechi za mzunguko wa nne jana.


MSImaMO LIGI KUU ENGLAND 2017/ 18




TimuPWDLGFGAGDPTS
1Man UtdMan Utd43101221010
2Man CityMan City4310102810
3ChelseaChelsea43018539
4WatfordWatford42207348
5TottenhamTottenham42117347
6HuddersfieldHuddersfield42114227
7BurnleyBurnley42115417
8LiverpoolLiverpool42118807
9West BromWest Brom42114407
10NewcastleNewcastle42024316
11ArsenalArsenal420278-16
12StokeStoke41214405
13SouthamptonSouthampton412134-15
14BrightonBrighton411235-24
15SwanseaSwansea411225-34
16EvertonEverton411226-44
17LeicesterLeicester410368-23
18West HamWest Ham4103410-63
19BournemouthBournemouth400418-70
20Crystal PalaceCrystal Palace400407-70

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...