![]() |
| Kylian Mbappe |
PARIS, Ufaransa
ARSENE Wenger anaamini Kylian Mbappe anaweza kuwa Pele (mchezaji wa zamani wa Brazil) ajaye katika soka baada ya kuhamia katika timu ya Paris Saint-Germain mkopo katika majira haya ya joto.
Wenger amesema haoni kama kuna ukomo wa umuhimu wa mchezaji huyo kinda.
Akizungumza na na kituo cha runinga cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot, Wenger alisema: “Mbappe anaweza kuwa Pele ajaye.
“Hakuna ukomo wa umbali ambao anaweza kwenda.”
Alisema: “ Pia nilimhitaji, lakini dau la euro milioni 180 ni kubwa mno kwetu. Amekuwa akicheza vizuri kama mshambuliaji.
![]() |
| Pele |
“Anafunga mabao na anatengeneza nafasi, Ni mchezaji mwenye ubora.
Mchezaji huyo wa Ufaransa, amehamia PSG katika siku ya mwisho ya dirisha la usajili kwa mkopo, inaweza kumsaini katika majira ya joto yajayo kwa ada ya pauni milioni 162.
Akiwa na miaka 18 alicheza kwa kiwango cha hali ya juu kwenye timu ya Monaco msimu uliopita, aliisaidia kutwaa ubingwa wa Ufaransa na kufika nusu fainali Ligi ya Mabingwa.
![]() |
| Arsene Wenger |
Katika msimu uliopita Mbappe aliifungia AS Monaco mabao 26 katika mechi 44 na kuchanguliwa kuichezea timu ya taifa.
Kutokana na kuwa na kiwango kizuri wakati wa uhamisho timu nyingi za Ulaya zilihusishwa na kumtaka ikiwemo Real Madrid na Arsenal.
Inajulikana Gunners ilituma ofa ya pauni milioni123 kwa ajili ya kumtaka Mbappe Julai mwaka huu.
Wenger pia alithibitisha kutuma ofa ya pauni milioni 91 kwa Monacco kwa ajili ya kumtaka Thomas Lemar katika siku ya mwisho ya usajili.



Comments
Post a Comment