![]() |
| Arsene Wenger |
ARSENE Wenger (67) amekiri kwa mara ya kwanza kwamba alikaribia kuondoka katika kiti cha ukocha mwanzani mwa mwaka huu, na sasa lazima ajutie uamuzi wake wa kutofuata dhamira yake.
Wenger aliiambia alikiambia kituo cha televisheni cha
Telefot cha ufaransa jana kuwa alisita kusaini mkataba mwingine Arsenal kutokana na kuwa na wasiwasi kama endelee kuwa kocha wa Gunners au la, kwa maoni hayo ina maana kuwa alikaribia kuacha kuinoa timu hiyo baada ya kuitumikia kwa zaidi ya miaka 20.
"Ndiyo, Nilisita kuongeza mkataba kwa sababu binafsi. Nimekuwa Arsenal kwa miaka 20, na ninajiuliza kama nitaendelea kuiongoza klabu. Tulikwenda vibaya sana katika msimu."
Katika msimu uliopita Wenger aliisaidia Arsenal kutwaa ubingwa wa saba wa Kombe la FA katika Uwanja wa Wembley Mei mwaka huu inawezekana ulichangia kuamua kuongeza mkataba mwaka mmoja.
Baada ya kuanza msimu huu vibaya, akishinda mchezo mmoja dhidi ya Leicester City mabao 4-3 kabla ya kufungwa bao 1-0 dhidi ya Stoke na mabao 4-0 dhidi ya Liverpool, Wenger amekuwa akijaribu kuwashawishi mashabiki kuwa na imani naye ili aendelee kuiongoza timu.
Wenger akizungumza na beIN Sport TV Ijumaa alikanusha kwamba klabu ilikuwa ikitaka kumuuza Alexis Sanchez kwa Manchester City katika siku ya mwisho ya uhamisho.
Arsenal ilijaribu kumsaini kiungo wa Monaco, Thomas Lemar katika siku ya mwisho ya uhamisho na kutuma ofa ya zaidi ya milioni 90 lakini ilimkosa.
Wenger kwa sasa yuko kwenye hatari ya kumkosa
Sanchez na Mesut Ozil katika majira ya joto yajayo kwa kuwa watakuwa wamemaliza mikataba yao huku
Alex Oxlade-Chamberlain akiwa amehamia Liverpool kwa ada ya pauni milioni 35.
Mashabiki wametishia kususia mechi ya Jumamosi wakati Arsenal itakapocheza na Bournemouth katika uwanja wa Emirates ikiwa ni sehemu ya kushinikiza Wenger aondoke.
Wachezaji wa zamani wa timu hiyo Wright na Martin Keow na wanaunga mkono kocha huyo aachie ngazi.
Wamiliki wa timu wamekuwa wakimuunga mkono Wenger kwa kuwa amekuwa akiifanya timu kujiendesha kwa faida.
Kocha wa Jose Mourinho United aliwahi kukejeli kuwa kocha pekee aliye kazini ambaye anafanya kazi bila ya kuogopa kutimliwa kwa timu kufanya vibaya ni Wenger.

Comments
Post a Comment