LONDON, Uingereza
TIMU za Liverpool na Manchester City na Chelsea zimekodi ndege maalumu kuwarejesha England wachezaji wao wanaochezea timu ya Brazil, Philippe Coutinho, Fernandinho, Gabriel Jesus, Ederson, Roberto Firmino na Willian.
Nyota wa Liverpool ni Coutinho na Roberto Firmino, Chelsea ni winga Willian na wa Manchester City ni Fernandinho, Gabriel Jesus na mlinda mlango Ederson.
Wachezaji hao wamechuliwa usiku wa jana kurejea Uingereza ili kucheza katika mechi za mwishoni mwa wiki za Ligi Kuu England.
Coutinho ambaye alikuwa na timu ya Brazil iliyocheza dhidi ya Colombia jana na kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya michuano ya kuwania kombe la Dunia 2018 anaweza kucheza mechi yake ya kwanza katika timu ya Liverpool msimu huu wakati itakapocheza Manchester City.
![]() |
Neymar (kulia) akiwa kwenye ndege ya kukodi kutoka Brazil kuelekea paridi Ufaransa akiwa an wachezaji wenzie (Lishoto kwenda kulia) Thiago Silva, Dani Alves, Filipe Luiz, Marquinhos na Jemerson
|
Pia Neymar aliondoka na timu nzima ya Brazil kabla ya kupanda ndege ya kukodi kurejea Ufaransa kwa ajili ya kuendelea na michezo ya ligi.
Nyota huyo wa PSG ametupia picha kwenye akaunti yake ya Instagram inayomwonesha akiwa pamoja na wachezaji wenzie katika timu moja Thiago Silva, Dani Alves na Marquinhos, pia mlinzi wa Atletico Madrid, Filipe Luiz na wa Monaco, Jemerson.
Klabu za Ulaya zimeshirikiana kulipa gharama za kukodi ndege ili kuwarejesha haraka wachezaji wao kwenye timu zao kwa ajili ya kuwatumia kwenye Ligi Kuu ya nchi zao na Ligi ya Mabingwa.


Comments
Post a Comment