Skip to main content

Tanzanite , Nigeria kazikazi leo


Mwandishi wetu
TIMU ya Tanzania ya soka ya wanawake umri chini ya miaka 20 leo itashuka uwanjani katika mji wa Benin City kupambana na wenzao wa Nigeria, Falconets katika mchezo wa kwanza wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Ufaransa.
Msafara wa timu ya tanzania wenye wachezaji 20 uliondoka Alhamisi usiku kuelekea Abuja on Thursday kabla ya kuunganisha safari kwenda Benin City kwa mchezo wa  leo.
Waamuzi waliochaguliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Afrika (CAF) kuchezesha pambano hilo ni Vincentia Enyonam Amedome wa Togo atakayekuwa katikati, akisaidiwa na
Kossiwa Kpadenou na Abra Sitsope Agbedanou huku Aissata Ameyo Amegee akiwa mwamuziki wa nne.
Kamishina na mechi ni Rochell Woodson kutoka Liberia.
Kabla ya kuondoka nchini kocha wa timu hiyo Sebastian Nkoma alisema wana matumaini ya kufanya vema kwenye mchezo wa leo huku nahodha wa timu hiyo, Wema Richard akisema wanatumiani kushinda na kurudi na ushindi , kauli mbiu yao ni “Hapa ni kazi kazi.”
Kikosi cha wachezaji 20 wa Tanzanite kilichoko Nigeria ambacho kutoka humo kocha Nkoma atachagua timu yake ya wachezaji 11 na wa akiba ni makipa watatuAgatha Joel, Zainab Abdallah na Gelwa Mgomba,  walinzi; Eva Jackson, Aquila Gasper, Asphat Kasindo, Ester Mayala, Silivia Mwacha,  Stella Wilbert, Wema Richard,  Hadija Ali, Rukia Anafi na Christine Daudi.
Viungo ni Herieth Shija, Julieth Singano na Shamimu Hamis na Washambuliaji ni Veronica Mapunda, Opa Clement, Zainabu Mohamed na Philomena Daniel.
Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika Oktoba Mos kwenye uwanja wa Chamazi.
Mshindi katika mechi mbili za timu hizo atapambana na
mshindi kati ya Morocco na Senegal katika mzunguko unaofuata Novemba mwakani.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...