| Mkuu wa Mkoa wa Mara Dk Charles Mlingwa(aliyevaa koti la suti) akicheza mziki wakati wa uzinduzi wa tamasha la Tigo Fiesta, kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma mkoani humo usiku wa kuamkia jana . |
Mwandishi Wetu, Mara
WAKAZI wa mji wa Musoma wamelipokea tamasha la Tigo Fiesta 2017 kwa furaha kubwa baada ya kulikosa mwaka jana.
Akifungua tamasha hilo, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dk. Charles Mlingwa alisema hiyo ni fursa ya pekee kwa tamasha hilo kufanyika mkoani mwao tena kwa upendeleo wa kuwa mkoa wa pili baada ya Arusha.
| Msanii wa nyimbo za kitamaduni Saida Karoli, akitumbuiza kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma Mkoa wa Mara,kwenye tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana . |
''Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru Tigo na Clouds Media kwa kutuletea fursa mkoani kwetu, najua wakazi wa Musoma mmefaidika sana kwenye biashara mbalimbali, naomba niwahakikishie leo mtaburudika na mtaondoka salama kwa ulinzi tuliweka, alisema Mlingwa.
Msanii Coyo aliamsha mashabiki waliofurika uwanja wa Karume mjini hapa kwa kupanda jukwaani na kuwafanya wapagawe na nyimbo zake akifuatiwa na Nandy.
Wasanii wa muziki wa rap Roma Mkatoliki na Stamina (Rostam) ndio waliibeba Tigo Fiesta vilivyo walipoimba pamoja ikiwemo wimbo wao mpya 'Huku au Kule' na kushangiliwa kwa nguvu na mashabiki.
| Roma Mkatoliki na Stamina wakifanya yao. |
Alisema Tigo imepeleka huduma za intaneti kwenye shule kadhaa ili kuwasaidia wanafunzi wa shule za sekondari kusoma kwa njia ya mtandao, ambayo imeanza kunufaisha shule mbalimbali
Kwa upande wa mashabiki Michael Joseph mkazi wa Tarime alisema aliamua kukusanya fedha kidogo kidogo ili aje aone tamasha hilo, amefurahi kutimiza dhamira yake kwa kuona wasanii mbalimbali wakitumbuiza.
Jumla ya wasanii 17 walipanda jukwaani wakiwemo
Nandy, Ditto, Benpol'Jux, Saida, Joh, Darassa, Roma, Blue, Fid Q, Stamina, Chege, Shilole, Dulla Makabila Adam Mchomvu, Coyo na Future.
Comments
Post a Comment