![]() |
| Sloane Stephens akifuarahi baada ya kukabidhiwa Kombe la Ubingwa wa tenisi kwa wanawake katika mashindano ya Marekani baada ya kumfunga kwa seti 2-0 Madison Keys kwenye uwanja wa Flushing Meadows. |
NEW YORK, Marekani
SLOANE Stephens amekuwa bingwa mashindano ya Tenisi ya Marekani 2017 kwa upande wa wanawake baada ya kumshinda kwa seti 2-0 mmarekani mwenzie, Madison Keys katika mchezo wa fainali uliochezwa Uwanja wa Flushing Meadows.
Stephens ambaye katika viwango vya ubora wa tenisi vya dunia anashikilia namba 83 alimzidi mpinzani wake wakati wote wa mchezo na kupata alama 6-3, 6-0 .
Kwa kutwaa ubingwa huo, ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza ambaye yuko chini kwenye viwango vya ubora kufika fainali na kutwaa ubingwa wa mashindano hayo. Kwa mara ya mwisho aliyefanya hivyo alikuwa ni Clijsters 2009 alitwaa ubingwa baada ya kujifungua na kuwa na mtoto.
![]() |
| Sloane Stephens (kushoto) akipongezana na Madison Keys baada ya mchezo kuisha. |
Stephens pamoja na kupata kombe 'ametajirika' kwa kupata zawadi ya pauni milioni 2.84 ambazo ni sawa na zaidi ya sh. bilioni 8.4.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alianza kucheza katika mashindano ya tenisi ya Wimbledon baada kutocheza msimu mzima uliopita kutokana na kupata ufa katika mguu wake.
Alitumia saa moja na dakika moja, kushinda mchezo wake wa fainali dhidi ya mpinzani wake Madison Keys ambaye pia ni rafiki yake.
Stephens, ambaye kabla ya kuwa namba 83 kwa ubora alikuwa namba 934 wiki tano zilizopita, alisema: Ni kitu cha kusisimua, nilifanyiwa upasuaji Januari 23 na kama kama angetokea mtu na kuniambia nitakuwa bingwa wa Tenisi Marekani ningesema haiwezekani.
Keys alimpongeza Sloane ambaye alimwelezea kwua ni rafiki yake wa karibu, kwa kutwaa ubingwa huo na kusema katika mchezo wa fainali hakucheza kwa kiwango chake kizuri, amefurahia ushindi wa mpinzani wake.
Hata hivyo kwa kuwa mshindi wa pili katika mashindano hayo hajaondoka mikono mitupu. Amepata kombe na fedha dola za Marekani, 1,825,000 ambazo wa fedha za Tanzania ni zaidi ya sh. bilioni 4.



Comments
Post a Comment