SIMBA baada ya kutoka suluhu dhidi ya Azam FC katika mchezo wake wa mzunguko wa pili, imerudishaa dozi yake ya kufunga mabao kwa kuilaza mabao 3-0 (kibajaji) Mwadui FC kweney Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Mshambuliaji wa Kiganda, Emmanuel Okwi alionesha umuhimu wake katika kikosi cha Simba kwa kufunga mabao mawili katika ushindi huo na kufanya afikishe mabao sita katika mechi mbili alizocheza.
Kwenye mchezo uliopita dhidi ya Azam, Okwi hakucheza kwa kutokuwa fiti baada ya kutoka kuitumikia timu yake ya taifa ya Uganda iliyokwenda kucheza dhidi ya Misri na kufungwa bao 1-0 katika mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia.
Katika Mchezo wa kwanza dhidi ya Ruvu Shooting iliyoshinda mabao 7-0. Okwi alifunga manne.
Okwi jana alifunga mabao hayo dakika ya saba baada ya kupata pasi kutoka Shiza Kichuya na jingine dakika 67 baada ya kuwatoka walinzi wa Mwadui.
Bocco ambaye amesajiliwa Simba msimu huu akitokea Azam FC, jana aliosha nyota yake kwa kufunga bao lake la kwanza zuri msimu huu kwenye timu hiyo, dakika ya 72, baada ya kumpiga chenga mlinzi wa Mwadui.
Kwa ushindi huo Simba imefikisha pointi saba na kuwa ya pili sawa na Azam FC iliyopo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo nyuma ya Mtibwa yenye pointi tisa baada ya kushinda michezo yake yote mitatu iliyoanzia nyumbani. Mwadui ina pointi tatu.
Katika mchezo ujao Simba itacheza ugenini Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza dhidi ya Mbao FC, Sptemba 21, mwaka huu huku mwadui ikiikaribisha Tanzania Prisons siku hiyo Uwanja wa Mwadui Complex.
Simba; Aishi Manula, Ally Shomari, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murshid, Salim Mbonde, James Kotei, Emmanuel Okwi, Muzamil Yassin/Jonas Mkude, John Bocco, Nicholas Gyan/Mwinyi Kazimotona Shiza Kichuya/Laudit Mavugo.
Mwadui FC; Arnold Massawe, Malika Ndeule, David Luhende, Revocatus Mgunga, Abdallah Mfuko, Razack Khalfan, Abdallah Seseme, Awadh Juma/Uwesu Ally, Evarist Mjwahuko, Gerald Mathias/Benedicto Mwampyate na Hassan Kabunda.

Comments
Post a Comment