![]() |
| Cristiano Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake aliyofunga usiku wa kuamkia leo. |
MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo amerejea kwa kishindo katika timu ya Real Madrid baada ya kutoichezea katika Ligi Kuu Hispania akitumikia adhabu ya kukosa mechi tano kutokana na hatia ya kumsukuma refa katika mchezo dhidi ya Barcelona kwa kuifungia mabao mawili katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Apoel Nicosia katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa, huku akiendelea kuvunja rekodi katika mashindano hayo .
Ronaldo aliifungia Real ambao ni mabingwa watetezi mabao hayo dakika ya 12 na 51, la kwanza akifunga kwa shuti la karibu na la pili kwa penalti.
Mlinzi Sergio Ramos alifunga bao la tatu kwa tiktak.
![]() |
| Iker Casillas |
Real Madrid imeshinda mchezo wake wa kwanza katika mashindano hayo ikicheza uwanja wa nyumbani kati ya mara 11 ilizocheza.
Cristiano Ronaldo ameweka rekodi ya kufunga mabao 55 nyumbani ambayo ni mengi kuliko mchezaji yeyote katika Ligi ya Mabingwa huku Lionel Messi akimfuatia kwa kufunga mabao 54.
Ronaldo pia amefunga penalti nyingi zaidi 12 katika mashindano huku Messi akifunga 11.
Kwa matokeo hayo timu ya Real inayonolewa na Zinedine Zidane imekuwa kinara katika Kundi H kwa tofauti ya mabao na Tottenham, ambayo iliifunga Borussia Dortmund mabao 3-1.
Timu ya Besiktas ya Uturuki imekuwa kinara katika Kundi G baada ya kushinda mabao 3-1 ugenini dhidi ya Porto.
Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, timu iliyofika nusu fainali katika mashindano yaliopita Monaco ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ngeni kwen ye mashindano hayo RB Leipzig.
Mlinda mlango wa Porto, Iker Casillas ameifikia rekodi iliyowekwa na mchezaji wa zamani wa Manchester United, Ryan Giggs kwa kucheza katika mashindano 19 na kucheza na timu nyingi 53, tofauti kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa.
Katika uwanja wa Anfield, Liverpool imejikuta ikishindwa kuibuka na ushindi baada Joaquin Correa kufunga bao la kusawazisha na kufanya Sevilla itoke sare ya mabao 2-2 dhidi ya wenyeji wao.
Pia katika mchezo huo, Liverpool ilipata penalti lakini lakini Roberto Firmino alipiga nje.
Wageni walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Wissam Ben Yedder , kabla ya Firmino na Mohamed Salah kufunga kwa upande wa wenyeji.
Katika mchezo huo, kocha wa Sevilla, Eduardo Berizzo alitolewa uwanja kwenda kuka ana mashabiki kutokana na kunyanganya mlinzi wa Liverpool, Joe Gomez mpira wakati wa kurusha.
Katika mchezo wa Kundi F, timu ya Manchester City ikiwa ugenini, ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi Feyenoord ya Uholanzi mjini Rotterdam.
Mabao ya City yalifungwa na Stones (dk. 2, dk 63), Agüero (dk.10) na Jesus (dk.25)
Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Shakhtar Donetsk iliifunga Napoli mabao 2-1.


Comments
Post a Comment