![]() |
| Kocha Kinnah Phiri (katikati) wakati alipokuwa kazini, akitoa maelekezo kwa wachezaji wa Mbeya City msimu uliopita. |
Mwandishi Wetu
WAKATI klabu ya Mbeya City FC ikisema imefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na mkataba na Mmalawi Kinnah Phiri, kocha huyo ameibuka amesema mkataba wake haujavunjwa (uko hai), utakuwa utavunjwa baada ya kulipwa fedha zake.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amoss Makalla aliingilia kati na kuwa msuluhisi wa mgogoro kati ya Mbeya City na kocha huyo aliyemwomba kumsaidia kutokana na kutolipwa malimbikizo ya mshahara wake na kutohudumiwa.
Katika taarifa yake, iliyotoka jana Klabu ya Mbeya City FC imesema imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na aliyekuwa kocha wake mkuu, Kinnah F. Phiri
Taarifa kamili ya Mbeya City iliyotolewa jana kwenye tovuti yake na Ofisa na Habari wake Shah Mjanja inasomeka;
Klabu ya Mbeya City FC leo tarehe 13.09.2017 imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na aliyekuwa kocha Mkuu wake Kinnah F. Phiri.
Kikao cha leo ulikuwa ni mwendelezo wa vikao kadhaa baina ya pande hizi mbili toka mwezi Julai mwaka huu. Baada ya majadiliano marefu pande zote mbili zimekubaliana kutoendelea na makubaliano yao ya hapo awali.
Sababu kubwa ni matokeo mabaya ya timu ya msimu uliopita 2016/2017 ambayo yameipunguzia klabu uwezo mkubwa wa kuhimili mahitaji yake ya msingi baada ya wadhamini waliotarajia kuingia kushindikana na wadhamini waliopo kupunguza kiwango cha udhamini wao kutokana na matokeo hayo yasiyoridhisha.
Klabu itatangaza kocha mkuu baada ya muda mfupi ujao ila kwa sasa timu itabaki chini ya usimamizi wa kocha msaidizi, Mohamed Kijuso.
Klabu inapenda kumshukuru Kocha Phiri kwa mchango wake muhimu katika timu yetu, itaendelea kuuthamini na kuukumbuka na inaamini Kocha Phiri ataendelea kuwa msaada katika maendeleo ya timu yetu kwani amekuwa sehemu ya familia yetu.
Hata hivyo akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari jana, Phiri alisema mkataba wake bado uko hai, walikubaliana City itafute kocha wa kusimamia timu kwa muda, mkataba wake utavunjwa pale atakapokuwa amelipwa malimbikizo ya mshahara na stahili zake nyingine ambapo kwa jumla ni takriban sh. milioni 40.
Alisema anataka alipwe fedha hizo, mkataba ukivunjwa ndipo atatafuta timu nyingine ya kuifundisha.
Alisema wamekubaliana alipwe fedha zake ndani ya kipindi miezi mitatu, kama hatalipwa yuko tayari kuomba Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (Fifa) limsaidie kitu ambacho kitafanya City kulipa fedha nyingi zaidi.
Phiri alisaini mkataba wa miaka miwili Februari 8, 2016 akichukua nafasi ya Meja Mstaafu, Abdul Mingange ambaye naye alichukua nafasi hiyo baada ya aliyekuwa kocha mkuu, Juma Mwambusi kuhamia Yanga kuwa kocha msaidizi wa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Hans Pluijm ambaye kwa sasa anainoa Singida United.
Sintofahamu ya mkataba huo, imekuja siku chache tangu Phiri agome kukifundisha kikosi cha Mbeya City kwa madai ya malimbikizo ya mshahara, huku Mbeya City wakionekana kutomjali kabisa.
Katika msimu huu, Mbeya City imecheza michezo miwili ambayo yote imeongozwa na Kocha msaidizi Mohammed Kijuso, ina alama 3 baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya Majimaji na kupoteza dhidi ya Ndanda FC.
Kuvunjwa kwa mkataba huo kunakuja siku chache toka Phiri agome kukifundisha kikosi cha Mbeya City kwa madai ya malimbikizo ya mshahara, huku Mbeya City wakionekana kutomjali kabisa.
Mpaka sasa Mbeya City imecheza michezo miwili ambayo yote Imeongozwa na Kocha msaidizi Mohammed Kijuso.
Katika michezo hiyo Mbeya City wamekusanya alama 3 baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya Majimaji, na kupoteza dhidi ya Ndanda FC.
Rekodi ya Phiri
Phiri alijiunga na City Februari 8, 2016 akitokea klabu ya Free State ya Afrika Kusini , ameiongoza City katika michezo 44, akishinda michezo 12, akifungwa 15 na kutoka sare 17, ilifunga mabao 47 na kufungwa 54.
Phiri alijiunga na City Februari 8, 2016 akitokea klabu ya Free State ya Afrika Kusini na ameiongoza Timu hiyo katika michezo 44, akishinda michezo 12, akifungwa 15 na kutoka sare 17 huku akifunga mabao 47 na kufungwa mabao 54.

Comments
Post a Comment