![]() |
| Neymar akionesha jezi yake siku alipotambulishwa PSG akitokea Barcelona ya Hispania. |
NEYMAR Santos amesisitiza amehama Barcelona kwenda Paris kwa matumaini ya kupata mafanikio kwenye Ligi ya Mabingwa.
Paris Saint-Germain katika dirisha la usajili lililopita imevunja rekodi ya Dunia kwa kumsajili nyota huyo wa Brazil kwa ada ya pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 598 na kumnyakua kutoka Uwanja wa Nou Camp, ikivunja mkataba wake.
Neymar anayepata kiasi cha pauni 500,000 kwa wiki amesema sababu kubwa iliyofanya ahamie PSG ni kutokana na kuona ina nafasi ya kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa.
Akiwa na Barcelona Neymar alitwaa mataji nane katika misimu minne akicheza pamoja na Lionel Messi na Luis Suarez katika sehemu ya ushambuliaji.
Leo atacheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi ya mabingwa awakiwa na PSG dhidi ya Celtic katika Uwanja wa Parkhead.
![]() |
| Neymar akifurahia moja ya bao alilofunga wakati alipokuwa Barcelona. |
Neymar (25), alisema: “moja ya sababu kubwa ya kujiunga na PSG ni kusaidia kuandika historia. Ligi ya Mabingwa, si tu taji tunalolitaka kuchukua, lakini taji muhimu sana.
“Lengo la msimu huu ni kujaribu kutwaa, hilo ni daraja ambalo kwa sasa klabu ipo. Ninaamini tunauwezo wa kutwaa ubingwa.
“Si tu kwamba tukwamba tuna ubora lakini tuna uzoefu, wachezaji ambao wanajua kitu gani cha kufanya ili kutwaa Ligi ya Mabingwa.
“Nimeshatwaa ubingwa wa mashindano hayo, Dani Alves ametwaa mara tatu, Thiago Motta ametwaa ubingwa akiwa na Barcelona na Inter, Angel Di Maria alitwaa ubingwa Real Madrid. Si tu tuna ubora, lakini uzoefu wa kweli.”
Kuhusu ada yake aliyolipiwa alisema yeye hahusiki na lolote, ni klabu zenyewe zilizokubaliana.


Comments
Post a Comment