Skip to main content

Ndoa ya Rooney, Coleen mashakani, mke atimka nyumbani

Wayne Rooney , Coleen wakati wa furaha

LONDON, Uingereza
MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amewaambia rafiki zake anahofia ndoa yake itavunjika baada ya mkewe Coleen kuwachukua watoto wao watatu na kuondoka nao.
Coleen (31) ambaye ni mjamzito wikiendi hii alipumzika na wazazi wake, baada ya Rooney kukamatwa na polisi na kushikiliwa kwa muda kutokana na kuendesha gari huku akiwa amelewa na alikuwa na mwanamke mwingine (mchepuko) aitwaye Laura Simpson.
Coleen, aliondoka kwenye nyumba yao na Rooney Jumamosi mchana na kuwasili kwenye nyumba ya familia yao akiwa na gari aina ya  Range Rover akiwa na watoto wake wa kiume Kai (7), Klay (4) Kit mwenye mwaka mmoja.
Aliondoa kwenye nyumba yao saa chache baada ya kurejea kutoka Majorca, Hispania mapumzikoni na kujua kuwa mumewe ambaye ni mshambuliaji wa Everton alitiwa mbaroni kwa kuendesha gari huku akiwa amelewa na kwenye gari lake alikuwa na mchepuko Laura Simpson (29) ambaye ni mmoja wa wanawake wenye tabia ya kwenda kwenye klabu za starehe mara kwa mara.
Chanzo kimesema: “ Coleen ameamua kukaa na wazazi wake wakati akipanga ni kitu gani cha kufanya, lakini kwa wakati huu anahisi ndoa yake na Rooney ya miaka tisa itakuwa imeisha.
“Mambo yanaweza kubadilika katika siku zijazo lakini kwa sasa anaona inatosha na imekwisha. Anahisi kudhalilishwa. Anapanga kuondoka.”
Habari nyingine zinadai kuwa Wayne (31) amewaambia rafiki zake anahofia ndoa yake ya miaka tisa imekwisha. Hajui afanye nini.
“Alishaomba radhi kwa Coleen kwa mambo mengi aliyofanya nyuma, lakini bado inaonekana kuwa ngumu. Amechanganyikiwa.”
Coleen alisema jana kuwa ataendelea kubakia na watoto wake kama yeye na Rooney watatengana.
Ameweka kwenye kwenye mtandao wake wa Instagramn picha ya watoto wake na kuandika: “Bila ya kujali niko wapi kila wakati watanifuata na ninatumaini itakuwa hivyo.”
Wazazi wa Coleen wamekataa kuzungumza na mkwe wao Rooney  ambaye ni nahodha wazamani wa England .
Rafiki wa karibu wa Rooney na ndugu zake nao hawajaonekana kuwa karibu naye.
Nyumba  ya Rooney na mkewe Coleen.

Coleen akiwa na Colette walikwenda nyumbani kwa Rooney,  Prestbury, Cheshire Ijumaa na Coleen alimcharukia Wayne kuwasili akikatisha mapumziko yake nchini Hispania baada ya kusikia kukamatwa kwa mumewe.
Awali wiki mbili zilizopita Coleen aliweka picha yake inamwonesha akiwa na Rooney katika  Instagram baada ya mume wake kutangaza kustaafu kuchezea timu ya taifa ya England.
Aliandika chini yake: “Hongera kwa uchezaji wa kusisimua England! Tunakupenda na tunajivunia sana wewe !”
Wayne na mchepuko Laura walikutana Alhamisi usiku katika baa ya Symposium, Wilmslow kisha walichukua taksi iliyowapeleka mahali alikopaki gari, kabla ya kuendesha umbali wa km 21 kuelekea nyumbani kwake.
Laura  amesema hakuna kitu kibaya alichofanya na nyota huyo.
Wakala wa Wayne, Paul Stretford aliwasili kwenye nyumba ya nyota huyo kuzungumza naye.

Laura Simpson

Mwaka 2010 wakati Coleen alipokuwa na ujauzito wa Kai, Wayne alidaiwa kufanya mapenzi na Jenny Thompson na Helen Wood ambao nao ni wanawake wanaojirusha kwenye klabu za starehe
Wayne anatakiwa kufika kwenye mahakama ya Stockport Septemba18 kujibu mashtaka ya kuendesha gari huku akiwa amelewa. 
Kocha wake katika timu ya Everton manager Ronald Koeman leo anatarajiwa kuzungumza naye. Anaweza kutozwa faini ya mshahara wa wiki mbili kiasi cha pauni 320,000 (zaidi ya sh milioni 928.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...