Skip to main content

Nadal bingwa Tenisi Marekani, azoa bilioni 8.4/-

Rafael Nadal

NEW YORK, Marekani
RAFAEL Nadal ametwaa ubingwa wa mashindano ya Wazi ya Marekani kwa mara ya tatu na taji lake la 16 katika mashindano makubwa ya kila mwaka 'Grand Slam' baada ya kumshinda Kevin Anderson wa Afrika Kusini katika mchezo wa fainali uliochezwa New York alifajili ya leo.
Mchezaji huyo namba moja kwa ubora duniani alishinda kwa seti 3-0, akipata alama 6-3 6-3 6-4 katika Uwanja wa Flushing Meadows.
Pamoja na kutwaa taji hilo, Nadal amepata zawadi ya fedha kiasi cha dola 3,700,000 ambazo ni sawa na sh. bilioni 8.4 za Tanzania huku mpinzani wake akipata bilioni 4.2 na kombe dogo.
Nadal mwenye umri wa miaka (31), kwa mwaka huu ametwaa mataji mawili ya Slam kwa mwaka mmoja ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 2013,  taji jingine la mwaka huu alitwaa katika mashindano ya Ufaransa.

Safari ya Nadali kabla ya kutwaa ubingwa wa tenisi Marekani mwaka huu ilikuwa kama ifuatavyo;

Mzunguko wa kwanza: Alimfunga Dusan Lajovic (Serbia) 7-6 (7-6) 6-2 6-2
Mzunguko wa pili: Alimfunga Taro Daniel (Japan) 4-6 6-3 6-2 6-2
Mzunguko wa tatu : Alimfunga Leonardo Mayer (Argentina) 6-7 (7-3) 6-3 6-1 6-4
Mzunguko wa nne: Alimfunga Alexandr Dolgopolov (Ukraine) 6-2 6-4 6-1
Robo fainali: Alimfunga Andrey Rublev (Russia) 6-1 6-2 6-2
Nusu Fainali: Alimfunga Juan Martin del Potro (Argentina) 4-6 6-0 6-3 6-2
Fainali: Alimfunga Kevin Anderson (Afrika Kusini) 6-3 6-3 6-4

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...