Skip to main content

Misri yafifiza matumaini ya Uganda Kombe la Dunia, pata msimamo makundi


Mshambuliaji wa Liverpool na Misri, Mohamed Salah (wapili kushoto) akisepa na kijiji cha wachezaji wa Uganda katika mchezo uliofanyika mjini Alexandria, Misri jana. Misri ilishinsda bao 1-0.

CAIRO, Misri
MSHAMBULIAJI wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah amefunga bao pekee dhidi ya Uganda, ambalo limefufua matumaini ya timu yake kufuzu fainali za kombe la Dunia 2018.

Kwa matokeo hayo Uganda italazimika kupambana kupata ushindi katika michezo miwili iliyobaki na kuombea Misri ipoteze kuweza kufuzu fainali hizo.

Misri ambayo haijafuzu fainali za Kombe la Dunia tangu mwaka 1990 inaongoza kundi E sasa ina pointi tisa, huku Uganda ambayo nayo wiki mbili zilizopita iliifunga Misri bao 1-0 lililofungwa na Emmanuel Okwi imebaki na pointi saba.

Nyota wa Liverpool, Salah alifunga bao hilo dakika ya sita baada ya Abdallah Said kupifa shuti na kuokolewa mlinda mlango Denis Onyango na mpira kumkuta mfungaji alioukwamisha wavuni.

Onyango baadaye aliokoa mpira uliopigwa na Said na Ramadan Sobhi na kuinyima nafasi Misri kupata bao la pili, huku safu ya ushambuliaji ya Uganda ikishindwa kuipenya ngome ya Misri iliyokuwa chini ya  mlinga mlango mkongwe Essam El Hadary mwenye umri wa miaka 44.

Kocha wa Misri raia wa Argentina, Hector Cuper anaweza kuivusha timu hiyo kwenda fainali za Kombe la Dunia kama atashinda mechi bili zilizosalia, mchezo wa nyumbani dhidi ya
Congo wa Oktoba 8 kwenda kucheza ugenini dhidi ya Ghana mchezo wa mwisho Novemba.

Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Ghana iliichapa Congo mabao 5-1 matokeo ambayo umafanya ifikishe pointi tano na kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo na Congo kuwa ya mwisho ikiwa na pointi moja huku ikiondoka katika mbio za kufuzu fainali hizo zitakazofanyika Urusi.

Uganda katika mechi zake mbili za mwisho itacheza dhidi ya Ghana Oktoba 7  kabla ya kwenda kwenda Congo kumalizia mchezo wa mwisho Novemba.

Matokeo mengine ya mechi zilizofanyika jana ni kama ifuatavyo;
Afrika Kusini 1 - 2 Cape Verde
Congo DR 2 - 2 Tunisia
Ivory Coast 1 - 2 Gabon
Burkina Faso 2 - 2 Senegal
Mali 0 - 0 Morocco
Algeria 0 - 1 Zambia

ZINGATIO: Timu itakayoongoza kila kundi baada ya kuchezwa mechi za mwisho itakuwa imefuzu michuano hiyo itakayofanyika Urusi.

MSIMAMO WA MAKUNDI AFRIKA KUWANIA KUFUZU kOMBE LA DUNIA 2018.

KUNDI A

NaTimu
PWDLGFGAGDPts
1Tunisia431073410
2DR Congo42119547
3Guinea410347-33
4Libya410338-53

KUNDI B

NaTimu
PWDLGFGAGDPts
1Nigeria4310103710
2Zambia42116427
3Cameroon403137-43
4Algeria401338-51

KUNDI C

NaTimu
PWDLGFGAGDPts
1Cote d'Ivoire42117347
2Morocco41306066
3Gabon412124-25
4Mali402219-82

KUNDI D

NaTimu
PWDLGFGAGDPts
1Burkina Faso41305326
2Cape Verde420246-26
3Senegal41215415
4Africa Kusini411256-14

KUNDI E

NaTimuPWDLGFGAGDPts
1Misri43015239
2Uganda42112117
3Ghana41216425
4Congo401339-61

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...