![]() |
| Floyd Mayweather akisikiliza swali kutoka kwa Awkward Puppets. |
NEW YORK, Marekani
BONDIA Floyd Mayweather amesema kuwa anawapenzi saba kwa kuwa anaona kuwa na mmoja na ni sawa na kukaribia kutokuwa naye.
![]() |
| Baadhi ya magari yanayomilikiwa na Floyd Mayweather. |
Mbabe huyo wa ngumu alisema hayo wakati akijibu swali la mtangazaji Diego lilikuwa likiulizwa ana kinyago kiitwacho Awkward Puppets, cha YouTube, mambo mengine aliyohojiwa ni kiasi gani cha fedha alizonazo benki.
Katika mahojiano, Mayweather alisema ana wapenzi wanawake saba na anamiliki magari ya kifahari 25 yaliyoko Las Vegas ,lipo Bugatti jekundu na Ferrari yan njano.
Mayweather pia amesema fedha alizopata katika pambano lake la mwisho dhidi ya Conor McGregor mwezi uliopita ni za mwisho kulizpatia ulingoni.
'' Pambano la mwisho ni lile nilikocheza, lile lilikuwa ni pambano la fedha,' Mayweather alisema na kuongeza anajua kuna watu watataka kupigana naye tena katika sayari nyingine.
Mayweather alifanya mahojiano hayo na Diego katika klabu yake ya usiku iliyopo Las Vegas, iitwayo Girl Collection (Mkusanyiko wa wanawake).
Alipoulizwa ana wanawake wangapi alijibu yeye si mwanaume mwaminifu wa kuwa na mwanamke mmoja.
''Nina wanawake wangapi? Pengine kama saba,'' Mayweather alisema.
'' Tunakwenda kula pamoja, baadhi husafiri pamoja. Kuwa na mmoja ni sawa na karibu kutokuwa naye.''
Kuhusu fedha, Mayweather alisema na fedha nyingi katika akaunti zake benki, zinaweza kuwa dola milioni 200 hadi milioni 300.
Mayweather anakadiriwa kupata dola milioni 100 katika pambano lake dhidi ya McGregor Agosti mwaka huu.
Alimtwanga kwa TKO katika raundi ya 10 na kumfanya mwamuziki kusimamisha pambano, hivyo kureka rekodi ya kushinda mapambano 50 bila ya kupigwa.






Comments
Post a Comment