LONDON, Uingereza
TIMU za Manchester United, CSKA Moscow, Paris Saint Germain, Bayern Munich, Chelsea, Barcelona na Sporting Lisbon zimeanza vema kampeni yake ya kuwania taji la Ligi ya Mabingwa hatua ya makundi kwa kushinda mechi za kwanza zilizopigwa usiku wa kuamkia leo
![]() |
| Wachezaji wa Chelsea wakishangilia moja yakati ya mabao 6-0 waliyoshinda dhidi ya FK Qarabag. |
Mshambuliaji Lionel Messi alifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 3-0 wa Barcelona dhidi ya Juventus katika mchezo uliopigwa usiku wa kuamkia jana.
Katika mchezo wa Barcelona dhidi ya Juventus ambayo katika mashindano yaliopita ilishika nafasi ya pili, uliochezwa Uwanja wa Nou Camp, Messi alicheza kwa kiwango cha juu, huku mchezaji mpya wa timu hiyo, Ousmane Dembele akicheza mechi yake ya kwanza ya michuano hiyo kwenye timu yake mpya.
Matokeo ya mechi zote zilizopigwa usiku wa kuamkia leo ilikuwa ni;
Benfica 1 CSKA Moscow 2
Manchester United 3 FC Basel 0
Celtic 0 Paris Saint Germain 5
Bayern Munich 3 RSC Anderlecht 0
Chelsea 6 FK Qarabag 0
Roma 0 Atlético Madrid 0
Barcelona 3 Juventus 0
Olympiakos 2 Sporting Lisbon 3


Comments
Post a Comment