Skip to main content

Man City, Man United zabanana kileleni, ziko sawa kila kitu



Wachezaji wa  Manchester United wakishangilia moja ya mabao yao dhidi ya Everton jana.

LONDON, Uingereza
USHINDI wa mabao 4-0 iliopata Manchester United dhidi ya Everton katika Uwanja wa Old Trafford  umeongeza presha dhidi ya Manchester City kileleni ambapo kwa sasa timu hizo ziko sawa kwa kila kitu.
Katika mchezo dhidi ya Everton, United ilifunga mabao matatu katika dakika sita za mwisho na kufanya kocha Ronald Koeman kuendelea kuwa kwenye presha ikiwa nafasi ya 18 kwenye msimamo na kuwa na pointi nne katika michezo mitano.

Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero akishangilia baada ya kufunga  bao kwenye mchezo dhidi ya Watford.

Antonio Valencia alifunga bao la kuongoza dakika ya nne kabla ya Henrikh Mkhitaryan, Romelu Lukaku na Anthony Martial (penalti) kufunga katika dakika sita za mwisho.
Awali Manchester City Jumamosi ilishinda mabao 6-0 ugenini dhidi ya Watford ikiwa ni kipigo cha pili mfululizo baada ya kuifunga Liverpool mabao 5-0 katika Uwanja wa Etihad.
City inayonolewa na Kocha Pep Guardiola hadi sasa ina pointi 13, imecheza mechi tano, imeshinda nne, sare moja , moja na haijapoteza, imefunga mabao 16 kufungwa mawili, tofauti ya mabao ni 14, iko sawa kila kitu na United ambayo ni hasimu wake katika mji mmoja.
 Everton, baada ya kufungwa mabao 4-0 dhidi ya United, inakuwa imefungwa mabao 12 katika mechi nne za mwisho za mashindano yote na kushindwa kufunga bao.
Timu hiyo imetumia pauni milioni 140 katika majira ya joto yaliopita kwa usajili, ilijiwekea malengo ya kumaliza katika timu nne za juu, kitu ambacho kinaonekana kinaweza kuwa kigumu kwa mwenendo wake wa sasa.

Ufuatao ni msimamo wa Ligi Kuu England baada ya mechi za mwishoni mwa wiki.

Msimamo Ligi Kuu England 2017/2018 

NaTimuPWDLGFGAGDPts
1Manchester City54101621413
2Manchester United54101621413
3Chelsea531185310
4Newcastle United53026429
5Tottenham Hotspur52217348
6Huddersfield Town52215328
7Burnley52216518
8Liverpool52219908
9Southampton52214408
10West Bromwich Albion52214408
11Watford522179-28
12Arsenal521278-17
13Stoke City512256-15
14Swansea City512225-35
15Leicester City511379-24
16Brighton & Hove Albion511347-34
17West Ham United5113410-64
18Everton5113210-84
19AFC Bournemouth510439-63
20Crystal Palace500508-80

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...