![]() |
| Wachezaji wa Man City walishangilia moja kati ya mabao 6-0 waliofunga dhidi ya Watford jana. |
LONDON, Uingereza
TIMU ya Manchester City baada ya kuifunga Liverpool mabao 5-0, imeonesha kuwa ni moto wa kuotea mbali kwa kuifunga Watford na mabao 6-0. na kuzidi kuongoza ligi kwa kufikisha pointi 13 baada ya kucheza mechi tano.
City inayonolewa na kocha Pep Guardiola ikicheza ugenini na ilipata mabao yake matatu kupitia kwa Sergio Aguero (dk. 27' dk. 31' dk. 81' ), Jesus (dk 37), Otamendi (dk.63) na Sterling (dk.89' pen).
Liverpool ikicheza nyumbani kwenye uwanja wake wa Anfied ilishindwa kutamba na kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Burnley.
Matokeo ya mechi nyingine jana yalikuwa
Crystal Palace 0 Southampton 1
Huddersfield Town 1 Leicester City 1
Newcastle United 2 Stoke City 1
West Bromwich Albion 0 West Ham United 0
Man City kwa sasa inaonekana kwua ndiyo timu yake fowadi kali zaidi katika Ligi Kuu England ikiwa imefunga jumla ya mabao 16 na kufungwa mawili katika mechi tano na kujikusanyia pointi 13.
Sergio Aguero ndite anaongoza katika Ligi Kuu England kwa kugunga mabao matano akifuatiwa na mwchezaji mwenzie kwenye timu moja Jesus mwenye mabao manRomelu Lukaku wa Man united na J. Vardy wa Leicester.
Sadio Mané wa Liverpool na Álvaro Morata wa Chelsea kila mmoja ana mabao mawili.
Timu inayofuatia ni Man United United ambayo ina pointi 10, lakini imecheza mechi nne na leo inapambana na Everton huku yenyewe ikiwa imefunga sita.
Timu inayoonekana kuwa na safu mbovu zaidi ya ulinzi hadi sasa ni West Ham United ambayo imefungwa mabao 10 na kufunga manne.
Ratiba za mechi za leo
Jumapili Septemba 17, 2017
Chelsea v Arsenal Stamford Bridge saa 09:30
Manchester United v Everton Old Trafford saa 12:00
Msimamo Ligi Kuu England
Na Timu P W D L GF GA GD Pts
1 Manchester City 5 4 1 0 16 2 14 13
2 Manchester United 4 3 1 0 12 2 10 10
3 Chelsea 4 3 0 1 8 5 3 9
4 Newcastle United 5 3 0 2 6 4 2 9
5 Tottenham Hotspur 5 2 2 1 7 3 4 8
6 Huddersfield Town 5 2 2 1 5 3 2 8
7 Burnley 5 2 2 1 6 5 1 8
8 Liverpool 5 2 2 1 9 9 0 8
9 Southampton 5 2 2 1 4 4 0 8
10 West Bromwich 5 2 2 1 4 4 0 8
11 Watford 5 2 2 1 7 9 -2 8
12 Arsenal 4 2 0 2 7 8 -1 6
13 Stoke City 5 1 2 2 5 6 -1 5
14 Swansea City 5 1 2 2 2 5 -3 5
15 Leicester City 5 1 1 3 7 9 -2 4
16 Brighton 5 1 1 3 4 7 -3 4
17 Everton 4 1 1 2 2 6 -4 4
18 West Ham United 5 1 1 3 4 10 -6 4
19 AFC Bournemouth 5 1 0 4 3 9 -6 3
20 Crystal Palace 5 0 0 5 0 8 -8 0

Comments
Post a Comment