![]() |
| Nyumba aliyoinunua Madonna. |
LISBON, Ureno
MWANAMUZIKI malkia wa pop, Madonna Louise Ciccon amenunua nyumba ya kifahari kwa pauni milioni 6.8 sawa na zaidi ya sh bilioni 20 za Tanzania, mjini Lisbon, Ureno ili kukaa na kumsapoti mwanaye aliyemwasili nchini Malawi, James Banda (11)amepata nafasi ya kucheza soka katika kituo cha klabu ya Benfica.
![]() |
| Madonna akiwa na David Banda |
David Banda amepata nafasi hiyo baada ya kufanyiwa majaribio na kuonekana kuwa na kipaji, Madonna ambaye amekuwa akifanya shughuli za muziki Marekani kwa kuwa hana matatizo ya fedha ameamua kununua nyumba Ureno ili kuachana na mambo ya kufikia hotelini anapokwenda kumwona mwanaye huyo.
Nyumba aliyonunua ni ya kizamani lakini nzuri, ilijengwa 1865, ina eneo la gereji ambalo gari nne zinaweza kuegesha na sehemu nyingine kwa ajili magari ya wageni kama 20, iko katika eneo la ekari tano, ina vyumba vinne vya kulaa, mabafu saba.
Nyumba hiyo ina ghorofa nne, iko katika eneo la Sintra, umbali wa maili 20 kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Ureno, Lisbon, imepakwa rangi ya machungwa.
Nyota huyo kwa sasa yuko nchini humo akiishi hotelini, katika miezi ya karibuni aliweka picha zake kwenye ukurasa wake wa mtandao Instagram zinazomwonesha akiwa mapumzikoni nchini Ureno.
![]() |
| Madonna akiwa na familia yake yote. |
Jarida la nchjini humo, Visao hizi karibuni liliandika habari, ''Madonna si mtalii, kwa sasa anaishi Lisbon" na yote hiyo ni kwa ajili ya kipaji cha mpira wa miguu cha mwanaye.
David, ambaye aliasiliwa na Madonna kutoka Malawi mwaka 2006 pamoja na Mercy James amejiunga na kituo cha soka cha Benfica kilichopo katika mji wa Seixal, uliopo nje kidogo ya jiji la Lisbon.
Atabakia katika kituo hadi atapoanza shule katika shule ya Kifaransa mjini Lisbon.
Banda ni mmoja kati ya watoto wanne wa Madonna aliowaasili Malawi baada ya Februari mwaka huu kupewa kibali mahakama ya nchini humo cha kuwaasili pacha. Pia ana watoto wawili wa kuwazaa mwenyewe.



Comments
Post a Comment