Picha iliyopigwa Aprili 2, 2013 ikimwonesha Madonna (wapili kushoto) akiwa na mwanaye wa kumzaa na aliowaasili (kuanzia kushoto kwenda kulia), David Banda, Lourdes, Mercy James na Rocco walipokuwa katika Shuke ya Msingi Mkoko iliyojengwa kwa kutumia mfuko wake na kushirikiana na taasisi ya ya Marekani BuildOn, katika Mkoa wa Kasungu, nchini Malawi. Mahakama ya Malawi Februari 7, 2017 ilitoa kibali kwa Madonna kuwaasili watoto wawili pacha wasichana, na kufanya idadi ya watoto aliowaasili kutoka nchini humo kuwa wanne.( PICHA NA AFP)
LISBON, Ureno
NYOTA wa muziki wa pop Madonna amehamia katika mji wa Lisbon, Ureno ili kuungana na mwanaye aliyemuasili kutoka nchini Malawi, David Banda ajiunge na shule ya mpira wa miguu (academy) ya timu ya Benfica, taarifa zimesema.
“Madonna si mtalii tena, kwa sasa anaishi mjini Lisbon,” Jarida la kila wiki la Visao limesema, na kuweka
![]() |
| David Banda alivyo sasapicha nyingi za nyota huyo mwenye umri wa miaka 59 ilizozichukua kwenye akaunti yake ya Instagram wakati alipokuwa akitembelea Ureno katika miezi kadhaa iliopita. |
David Banda ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 11 amekubaliwa na timu ya Benfica kuendeleza kipaji chake kwenye shule yao ya soka iliyopo katibu na mji wa Lisbon.
Madonna amekuwa akiishi hotelini, lakini ameshanunua nyumba katika kijiji cha Sintra, kilichopo kiasi cha km 30 kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa Ureno.
Nyumba hiyo iliyojengwa karne ya 19 awali ilikuwa ikiizwa kwa dola milioni 9 ( zaidi ya sh. bilioni 20) na inaweza kuchukua miezi sita kukarabatiwa, kwa mujibu wa Visao.
Banda aliyeasiliwa na Madonna nchini Malawi 2006, amekwua akifanya mzoezi kwenye kituo cha Benfica kilichopo nje kidogo ya jiji la Lisbon katika eneo la Seixal, limeripoti gazeti la Correio da Manha .
Klabu huyo imekubali kumchukua mtoto huyo baada ya kumfanyia majaribio na kuridhika na kiwango chake, atabakia kwenye kituo hivho hadi atapoanza shule katika shule ya sekondari ya kifaransa iliyopo Lisbon, limesema gazeti la Correio da Manha, ikikariri habari hiyo kutoka katika chanzo kilichopo Benfica.
Banda ni mmoja kati ya watoto wa nne walioasiliwa na Madonna kutoka nchini Malawi baada ya kuwaasili wasichana pacha Februari mwaka huu. Pia ana watoto wawili wa kuwazaa mwenyewe.
Madonna si nyota wa kwanza kuhamia Lisbon, Ureno. Wengine ni nyota wa filamu, John Malkovich, Monica Bellucci na Michael Fassbender .


Comments
Post a Comment