Skip to main content

Joshua: Ronaldo atamtwanga Messi ulingoni


Lionel Messi katikati akimtoka Ronaldo Kushoto katika moja ya mechi zilizoikutanisha timu za barcelona na Real Madrid.

LONDON, Uingereza
BONDIA bingwa wa ngumi uzito wa juu duniani, Anthony Joshua amesema kama Cristiano Ronaldo angepanda ulingoni kutwangana na Lionel Messi angemshangilia Ronaldo kwa kuwa yuko vizuri kimwili kutokana na mazoezi.
Ronaldo na Messi  ni mahasimu wanaochezea timu hasimu za Rel Madrid na Barcelona na wamekuwa wakishindana na kubadilishana tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka katika miaka tisa iliyopita. 

Anthony Joshua

Nyota wa Barcelona, Messi anaongoza kwa kutwaa tuzo mara tano
huku Ronaldo akitwaa mara nne, Joshua anaamini kama wakipanda ulingoni ni Ronaldo atamtwanga Messi.
Joshua  aliiambia YouTube channel COPA90: 'Messi anaweza kukwepa lakini Ronaldo anaonekana kuwa na mapigo kama ya Bruce Lee!
'Unajua ninachomaanisha, unakaa mbali na akinyoosha mkono mmoja unakwisha. Messi kidogo anaonekana kama lilivyo jina lake 'uchafu kitu kilichovunjika,' alisema.
Bingwa huyo wa dunia wa  mikanda ya WBA na  IBO, pia alisema anafurahishwa na jinsi Ronaldo anavyopenda kazi yake, anavutiwa na historia yake ya kujituma na kujitangaza mwenyewe kwa kazi yake .
'Nimekuwa katika ngumi za kulipwa sasa kwa miaka mitatu, ninafikiri  mwanzoni nilikuwa nikijaribu kufanya kila kitu katika ngumi ili kuwa mchezaji wa kulipwa,' Joshua alisema. 
'Kumbuka sikuwa nafahamika sana, kwa hiyo nilitakiwa kujitambulisha kwa dunia, kwa hiyo katika miaka mitatu niliweza,  kujitangaza na kujitangaza.
'Kwa sasa niko katika daraja ambalo nilikuwa ninataka, sasa ninataka kuweka mtazamo wangu kuwa mpiganaji bora zaidi, nimehamasishwa na  Ronaldo,' alisema
Joshua pia amesema kama angeambiwa achague mwanasoka ambaye angependa kupigana naye angemchagua kiungo wa Manchester City, Yaya Toure kwa kuwa ukali wake ni kama dubwi'. 
Joshua kwa sasa anajiandaa kutwangana na mpiganaji wa Bulgaria, Kubrat Pulev Oktoba 28  mwaka huu Cardiff katika mbapambano la kuunganiosha mikanda mitatu ya IBF, WBA na IBO.
Ronaldo alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2016  na kuonekana anaweza kutetea  taji hilo 2017 baada ya kuisaidia Madrid  kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa na La Liga.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...