| Bondia Mtanzania Omari Kimweri 'Lion Boy 'katikati akiwa na mkewe Lawaridi Kimweri, kushoto ni kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' wakati wa sherehe ya ndoa yao . |
| Bondia Omari Kimweri 'Lion Boy akiwa na mkewe Lawaridi Kimweri . |
| Wageni wakicheza muziki. |
| Omari Kimweri 'Lion Boy ' na mkewe Lawaridi Kimweri wakichukua chakula . |
| Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa na msanii wa kundi la Segere Siza Mazongela wakati wa Sherehe ya bondia Omari Kimweri |
Mwandishi Wetu
BONDIA Mtanzania Omari Kimweri 'Lion Boy 'anayefanya shughuli zake nchini Australia ameachana na ukapera na kumwoa, Lawaridi Kimweri huku sherehe ikifanyika Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Vijana .
Akizungumza katika sherehe hiyo, Kimweri alisema ameamua kuoa ili kujenga familia yake , tofauti na watanzania wengine wanaokwenda Ulaya ambao huwa hawakumbuki nyumbani baada ya kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na wanzungu .
Ameamua kuoa nyumbani kwa kuwa amezaliwa Tanzania na kule anafanya kazi tu, hivyo amerudi nyumbani kuoa ili kuanzisha familia yake, kwani Mwafrika akioa mzungu mtoto huwa siyo wake huwa na rangi ya kizungu.
Kimweri aliongeza amekuja nchini na ujumbe wa watu wannekwa ajili ya arusi yake pamoja na kufanya utalii katika vivutio mbalimbali ambapo watatembelea mbunga za wanyama ya Serengeti, Mikumi pamoja na Zanzibar .
Bondia huyo kwa sasa amejikita katika kufanikisha Tanzania inakuwa juu katika mchezo wa masumbwi kupitia wafadhili wake pamoja na kazi anazozifanya akiwa huku, ameshaleta vifaa mbalimbali vya mchezo wa masumbwi kwa ajili ya kuwasaidia mabondia wa nchini
Comments
Post a Comment