Skip to main content

Hanover 96 yaongoza Bundesliga

Wachezaji wa Hanover 96 wakishangilia.

BERLIN, Ujerumani
TIMU mpya iliyopanda daraja katika Ligi Kuu ya Ujerumani, Hanover 96 imeongoza Ligi baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hamburg katika uwanja wa HDI-Arena, Hanover na kuwa juu ya timu za Dortmund na Hoffenheim.

Timu hizo zilikuwa sawa kwa pointi kila moja ikiwa na pointi saba kuelekea wikiendi ambapo Dortmund itacheza na Cologne na Hoffenheim itapambana na Hertha Berlin Jumapili.

Bao la Martin Harnik ndani ya dakika 60 na shuti la karibu la mchezaji aliyetokea benchi Ihlas Bebou katika dakika 81 yalifanya Hanover kupata ushindi wa mabao 2-0 na kuendeleza rekodi yake kwa kutofungwa katika mechi 16 za mashindano yote.

Mabingwa watetezi Bayern Munich wako nafasi ya sita kabla ya mchezo wao dhidi ya Mainz 05 leo.

Ratiba ya mechi za leo na kesho ni kama ifuatavyo;

Jumamosi Septemba 16, 2017
Eintracht Frankfurt v Augsburg Commerzbank-Arena saa 10:30
Stuttgart v Wolfsburg Mercedes-Benz-Arena                       10:30
Werder Bremen v Schalke 04 Weserstadion                       10:30
Bayern Munich v Mainz 05 Allianz-Arena                               10:30
RB Leipzig v Borussia M'gladbach Red Bull Arena                 1:30

Jumapili Septemba 17, 2017
Hoffenheim v Hertha BSC Wirsol Rhein-Neckar-Arena        08:30
Bayer Leverkusen v Freiburg BayArena                                10:30
Borussia Dortmund v Koln Signal-Iduna-Park                         1:00




Msimamo wa Bundesliga 2017/2018

NaTimuPWDLGFGAGDPts
1Hannover 96431051410
2Borussia Dortmund32105057
3Hoffenheim32105237
4RB Leipzig32016336
5Schalke 0432015236
6Bayern München32015326
7Hamburger SV420245-16
8Augsburg31115324
9Borussia M'gladbach31113304
10Hertha BSC31113304
11Eintracht Frankfurt31111104
12Wolfsburg311124-24
13Mainz 0531023303
14Stuttgart310225-33
15Freiburg302114-32
16Werder Bremen301214-31
17Bayer Leverkusen301248-41
18Köln300317-60



Comments