![]() |
| Ousmane Dembele |
BARCELONA, Hispania
TIMU ya Barcelona imethibitisha mchezaji wake iliyomsaini kwa ada iliyovunja rekodi ya Dunia,Ousmane Dembele atakaa nje ya uwanja kwa minne kutokana na kuumia goti katika mchezo walioshinda ugenini dhidi ya Getafe.
Dembele mwenye umri wa miaka 20, atasafiri kwenda Finland wiki hii na kufanyiwa upasuaji.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa aliumia katika mchezo wake wa kwanza katika La Liga katika Uwanja wa Coliseum Alfonso Perez na kulazimika kutoka uwanjani dakika ya 25.
Awali miamba hiyo ya Catalan ilitumaini alikuwa ameumia nyama za paja na angekaa nje kwa wiki chache, lakini vipimo alivyofanyika Jumapili vimetoa matokeo ambayo hayakutarajiwa, ameonekana kuumia zaidi.
" Vipimo vimethibitisha kwamba mchezaji wa timu ya kwanza Ousmane Dembele alichanika katika mshipa uliopo nyuma ya paja la mguu wa kushoto," Barca imesema taarifa.
"Mchezaji atafanyiwa upasuaji na Dk. Sakari Orava nchini Finland wiki hii. Anatarajiwa kuwa kuwa nje kwa miezi mitatu na nusu na miezi minne."
Baada ya kuondoka kwa Neymar katika timu ya Paris Saint-Germain kwa ada ya pauni milioni 198 zaidi ya bilioni 500, Barca ilitumia sehemu ya fedha hizo kumsaini Dembele kutoka Borussia Dortmund, huku mchezaji huyo wa zamani wa Rennes akimzidi Luis Suarez kuwa mchezaji aliyesainiwa kwa ada kubwa zaidi kwenye klabu.
Barca ililipa euro milioni 105 (sh. bilioni 28) kwa kumsaini Dembele, kulingana na mkataba italazimika kuongeza fedha nyingine na kufikia euro milioni 145 (zaidi ya sh. bilioni 388.5) kulingana na uchezaji wake katika Ligi na mashindano ya Ligi ya Mabingwa
Awali Dembele alichezea mechi ya kwanza Barca, akitokea benchi wiki iliyopita ambapi timu yake ilishinda dhidi ya Espanyol, na kutengeneza bao la tano kwa Luis Suarez.
Kocha wa Barca, Ernesto Valverde kisha alimwanzisha kwenye mchezo wa Ligi ya mabingwa dhidi ya Juventus katikati ya wiki iliyopita.
Kutokana na kuumia kwake, Dembela atakaa nje ya uwanja hadi mwakani, anatarajiwa kucheza mchezo wa kwanza ugenini dhidi ya Getafe.
Pia Barca haitakuwa na mchezaji huyo katika mechi zote la Ligi ya Mabingwa hatu ya makundi, na pambano la kwanza la Clasico dhidi ya Real Madrid,Desemba 23, mwaka huu.
Kutokana na kuumia kwa Dembele kutafanya mchezaji mmpya mwingine kwenye timu hiyo
, Gerard Deulofeu kupigania kuingia kwenye timu ya kwanza.
Deulofeu alirejea Barca akitokea Everton kwa ada ya pauni euro milioni 12, lakini baada ya kuwasili kwa Dembele kocha Valverde alikuwa akimtumia pamoja na Lionel Messi na Suarez.
Wachezaji wengine ni wanaocheza nafasi yake ni Paco Alcacer, Denis Suarez na Arda Turan.

Comments
Post a Comment