Skip to main content

Barcelona, Juve, Man United, Munich vitani Ligi ya Mabingwa


MADRID, Hispania
KINYANG'ANYIRO cha Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi kinaanza leo na kesho kwa kuzikutanisha timu 32, leo zikianza 16 katika viwanja nane tofauti. Mechi zote zitaanza saa 3:45 usiku

Leo msisimko mkubwa kwa mashabiki ni mchezo wa Kundi D kati ya Barcelona dhidi ya Juventus kwenye Uwanja wa Nou Camp huku timu za Olympiakos na Sporting Lisbon nazo zikipambana  kuwania pointi tatu.

Barcelona inayonolewa na Ernesto Valverde itaikaribisha Juventus huku ikionekana katika miaka ya karibuni zikiwa na upinzani katika msimu huu tayari zilikutana katika mashindano ya kuwania Kombe la Kimataifa,  ambapo  Barca ilishinda mabao 2-1, yote (kwa  Barca) yalifungwa na Neymar.

2015 timu hizo zilikutana katika fainali ya mashindano hayo Barca kutwaa ubingwa, lakini Juve ililipa kisasi walipokutana katika robo fainali msimu uliopita kwa kupata ushindi wa mabao 3-0 kwa ujumla na kutinga nusu na fainali.

Barca imempoteza Neymar aliyehamia PSG ya Ufaransa lakini itakuwa na Ousmane Dembele iliyomsaini kama mbadala wake kutoka Borrusia Dortmund ya Ujerumani, ambaye ameonesha uwezo mkubwa katika ligi.

Valverde ambaye timu yake imeshinda mechi zake zote tatu katika La Liga na kuongoza kwa pointi tisa, leo atamkosa Arda Turan ambaye ni majeruhi, anaweza kuwa na kiungo Ivan Rakitic,  anajivunia safu yake ya ushambuliaji yenye wachezaji kama Lionel Messi, Luis Suarez, Dembele na Deulofeu.

Kwa upande wa Juve itakayoongozwa na mlinda mlango mkongwe Gianluigi , safu yake ya ushambuliaji inatarajiwa kuwa na Higuain, Dybala na Mandzukic ambao wameisaidia timu hiyo kufanya vizuri katika Ligi Kuu ya Italia, Serie A ikishinda mechi tatu za mwanzo na kuongoza kwa kuwa na pointi tisa sawa na timu za, SSC Napoli, na
na Inter Milan.

Mchezo mwingine utakaovuta hisia ni kati ya Manchester United  dhidi ya FC Basel wa Kundi A kwenye Uwanja wa Old Trafford, Uingereza.

Mashabiki watataka kuona kama United inayonolewa na Kocha Jose Mourinho itaonesha makali yake kama katika Ligi  Kuu England, ilipofunga mabao nane katika mechi mbili za mwanzo kabla ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Stoke mwishoni mwa wiki.

Mchezo mwingine wa kundi hilo utazikutanisha timu za Benfica  dhidi ya CSKA Moscow.

Katika Kundi B, Celtic inayonolewa na Brendan Rodger itapambana na Paris Saint Germain itakayokuwa na washambuliaji wake wapya, Neymar na Kylian Mbappe iliowasaini katika majira haya ya joto kwenye uwanja wa
Parkhead .
Je, Celtic inaweza kuisimamisha PSG nyumbani kama ilivyowahi kuifanyia Manchester City msimu uliopita kwa kutoka nayo sare ya mabao 3-3 ? Hilo ni swali ambalo jibu lake litapatikana baada ya dakika 90.
Mchezo mwingine wa kundi hilo utaikutanisha
Bayern Munich dhidi ya RSC Anderlecht.
Katika Kundi C, Chelsea itakuwa mwenyeji wa FK Qarabag na Roma itaikaribisha Atlético Madrid.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...