![]() |
| Ibrahim Ajibu katikati, |
BAO pekee zuri lililofungwa Ibrahim Ajibu dakika ya 16 limeamua matokeo kati ya Yanga ambao ni mabingwa watetezi Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya wenyeji wa Njombe Mji kwenye Uwanja wa Saba Saba mjini Njombe.
Kwa ushindi huo, Yanga imefikisha pointi nne sawa na timu za Simba na Azam FC baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Lipuli ya Iringa kwenye mchezo wa kwanza nyumbani, Dar es Salaam.
Hata hivyo Mtibwa Sugar ndiyo kinara wa Ligi hiyo baada ya kuifunga Mwadui bao 1-0 hivyo kufikisha pointi sita baada ya kushinda mchezo wao wa kwanza dhidi ya Stand United.
Ajib alifunga bao hilo dakika ya 16 mpira wa adhabu akipiga shuti la umbali wa meta 30, baada ya kuangushwa kwake.
Yanga, walitawala vizuri mchezo kipindi chote cha kwanza na wapinzani wao kucheza vizuri kipindi cha pili lakini mlinda mlango wa Yanga, Youthe Rostand alikuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi.
Matokeo ya mechi nyingine jana, Singida United ilishinda mabao 2-1 Mbao FC, Kagera iligawana pointi na Ruvu Shooting kwa kufungana bao 1-1, Ndanda iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City na Lipuli iliifunga Stand United bao 1-0.
Njombe Mji; David Kisu, Agaton Mapunda, Remmy Mbuligwe, Laban Kamboole, Peter Mwangosi, Joshua John, Awadh Salum, Hassan Kapalata/Behewa Sembwana, Notikeli Masasi, Ditrim Nchimbi na David Nakpa/Raphael Siame.
Yanga SC; Youthe Rostand, Juma Abdul, Gardiel Michael, Andrew Vincent, Kevin Yondan, Papy Kabamba Tshishimbi, Juma Mahadhi, Thabani Kamusoko/Raphael Daudi, Donald Ngoma/Obrey Chirwa , Ibrahim Hajib na Emmanuel Martin/Yussuf Mhilu.

Comments
Post a Comment