Skip to main content

Azam yafurahia kucheza Chamazi na Simba, Yanga

Uwanja wa Azam Complex

Mwandishi wetu

TIMU ya Azam FC imefurahia uamuzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwaruhusu kuutumia uwanja wao wa Azam Complex uliopo Chamazi kwa mechi zake zote za nyumbani za Ligi Kuu Tanzania ikiwemo dhidi ya Yanga na  Simba . 
Kwa mara ya kwanza vigogo vya soka nchini, Yanga na Simba zitacheza katika uwanja wa Azam Complex, unaomilikiwa na Azam FC, iliyoanzishwa mwaka 2007.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja wa Azam FC, Philipo Alando alisema wamefurahia kupata fursa ya kuutumia uwanja wao wa nyumbani kitu walichokuwa wanakililia.
“Ni jambo jema, tunafurahi kuona TFF hii inatoa makandokando yote ambayo yalikuwa magumu kufanyika huko awali, kama kuruhusu uwanja huu wa Chamazi kutumika kwa michezo yote.
Mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba ndio watakuwa wa kwanza kuandika historia ya kucheza na Azam FC kwenye uwanja huo katika mchezo wa Ligi Kuu ta Vodacom, Jumamosi hii.
Kwa upande wa mabingwa watetezi ligi hiyo, Yanga itashuka Chamazi Complex kuwavaa Azam katika mchezo wa mwisho wa kufunga mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo, Desemba 29 mwaka huu.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya kikosi kazi, kilichopewa kazi maalumu ya kupitia upya ratiba iliyokuwa imeandaliwa awali kuifanyia marekebisho, kumaliza majukumu kazi yake juzi na kutoa ratiba mpya inayoonesha uwanja huo kuanza kutumika kwa michezo mikubwa na miamba hiyo.
Uamuzi huo umefanywa na uongozi mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ulioingia madarakani Oktoba 12, mwaka huu tofauti wa awali uliotoa msimamo kuwa timu za Simba na Yanga zina mashabiki wengi hivyo uwanja huo ni mdogo (unaingiza mashabiki wachache 7,000) hivyo kutokuwa salama.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...