Skip to main content

Argentina hali tete kufuzu Kombe la Dunia, cheki msimamo

Mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi (kulia) akisikitika baada ya Venezuaele kupata bao.

BUENOS AIRES, Argentina
MBIO za Argentina kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi zimeendelea kusuasua baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu kibonde kwenye kundi lake Venezuela ambayo nji ya mwisho.
Venezuela  wakicheza ugenini walipata bao la kuongoza kupitia kwa Jhon Murillo lakini bao la kujifunga la kipindi cha pili liliipatia pointi moja Argentina.
Kwa matokeo hayo Argentina imeendelea kubaki katika nafasi ya tano kati ya sita huku zikiwa zimesalia mechi mbili, timu nne ndizo zitafuzu moja kwa moja huku ya tano italazimika kucheza mechi ya mchujo dhidi ya New Zealand na itakayoshinda itafuzo fainali hizo.
Katika mchezo mwingine wa kundi hilo la nchi za Marekani ya Kusini, Brazil ambayo imeshafuzu fainali hizo ilitoka sare ya bao 1-1dhidi ya Colombia.
Mshambuliaji wa Chelsea, Willian aliifungia bao la kwanza Brazil kabla ya mshambuliaji wa Monaco, Radamel Falcao kufunga la kusawazisha. 
Ushindi wa wa Uruguay wa mabao 2-1 dhidi ya Paraguay umeifanya timu hiyo kushika nafasi ya pili, huku Peru ikiichapa Ecuado na kutinga nafasi ya nne. Timu ya sita kwenye msimamo Chile ilichapwa bao 1-0 dhidi ya Bolivia.
Chile, inazidiwa pointi moja na Argentina, katika mchezo ujao itapambana na Ecuador kabla ya kwenda ugenini kucheza na Brazil katika mchezo wa mwisho.
Argentina iliyo na pointi sawa na Peru, katika mchezo ujao itakwenda kucheza na Ecuador. Mchezo wa mwisho wa Peru utakuwa dhidi ya Colombia.
Katika Kundi la Shirkisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Marekani ya Kaskazini, Kati na Caribbean (CONCACAF) Marekani ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Honduras. 
Timu zote mbili zina pointi tisa baada ya kucheza mechi nane huku Marekani ni ya nne na  Honduras ya tano.  timu tatu za juu zitafuzu moja kwa moja Kombe la Dunia.
Timu ya pili Costa Rica ilishindwa kujihakikishia nafasi Urusi baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Mexico ambayo imeshafuzu.
Panama imekuwa ya tatu kwa kuifunga Trinidad na Tobago 3-0.
Hadi sasa nchi ambazo tayari zimefuzu fainali hizo ni UbelgijiBrazilMexicoIranJapan, Jamhuri ya Korea na Saudi Arabia


Msimamo wa Kundi la nchi za CONCACAF

Na
Timu
P
W
D
L
GF
GA
GD
Pts
1
8
5
3
0
11
3
8
18
2
8
4
3
1
12
5
7
15
3
8
2
4
2
7
5
2
10
4
8
2
3
3
12
11
1
9
5
8
2
3
3
9
16
-7
9



Msimamo wa Kundi la Nchi za Marekani ya Kusini

NaTimuPWDLGFGAGDPts
1Brazil16114138112737
2Colombia167541916326
3Uruguay157352617924
4Peru167362625124
5Chile167272423123
6Argentina156541514123
7Paraguay156361621-521
8Ecuador166282424020
9Bolivia1641111434-2013
10Venezuela1514101734-177

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...