MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga wameibuka wabebe mbele ya
Singida United kwa kuifunga mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki.
Mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam jana, ulihudhuriwa na mashabiki wengi waliotaka kuona vikosi vya timu zote na kutokuwa na mechi muda mrefu.
Yanga ambayo imecheza mchezo huo ikiwa imetoka kwenye kambui yake Morogoro ilianza kupata bao dakika ya 5 ya likifungwa na Thaban Kamusoko.
Singida United ambayo imepanda daraja msimu huu imesawazisha dakika tatu baadaye kupitia kwa Danny Usengimana, baada ya kupokea pasi kutoka kwa Deus Kaseke ambaye katika msimu iliopita aliichezea timu hiyo ya Jangwani.
Singida United inayonolewa na Kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm ilipata bao la pili dakika ya 22 lililofungwa na mshambuliaji wake Simbarashe Nhivi na kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-1.
Mabadiliko yaliyofanywa na Yanga kipindi cha pili yaliinufaisha timu hiyo, walimtoa Emmanuel Martin, Mahadhi na Maka Edward na kuingia Donald Ngoma, Ibrahim Ajibu na Pius Buswita.
Yanga inayonolewa na kocha Mzambia George Lwandamina ilipata bao la pili na la kusawazisha kupitia kwa Amiss Tambwe kwa penalti baada ya Mlinda mlango wa Singida kumchezea vibaya, Aaid Ronaldo.
Huku mashabiki wakiamini kuwa mchezo huo ungeisha kwa sare, dakika ya 90, Yanga ilipata bao la tatu kupitia Emmanuel Martin kwa shuti kali na kuwafanya mashabiki wa timu yake kutoka na kicheko uwanjani.
Yanga imeutumia mchezo huo kwa maandalizi ya wamchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba Agosti 23 mwaka huu, pamoja na ligi
Comments
Post a Comment