| Wachezaji wa Yanga wakipasha miili |
Mwandishi wetu
WAKATI Simba ikikumbuka kwenda Morogoro kuweka kambi yake iliyoitumia kwa miaka miwili mfululizo kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga nayo itaweka kambi Pemba mahari imekuwa ikienda kujiandaa kwa pambano dhidi yamahasimu wao hao.
Yanga na Simba zinatarajiwa kupambana kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam Agosti 23, mwaka huu katika mchezo wa Ngao ya Jamii ambao ni ishara ya uzinduzi wa Ligi Kuu ya Vodacom.
Kabla ya kwenda Pemba, Yanga ambao ni mabingwa wa watetezi wa Ligi Kuu waliweka kambi ya zaidi ya siku 10 Morogoro, kisha kurejea Dar es Salaam na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Singida United na kupata ushindi wa mabao 3-2
Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten alisema timu hiyo itaweka kambi Pemba kuanzia Jumatatu ijayo sehemu ambayo uongozi umeona inafaa ili kuwafanya wachezaji kuwa na utulivu chini ya Kocha wao Mzambia, George Lwandamina kujiandaa na kurejea siku moja kabla ya pambano.
Comments
Post a Comment