MISS Tanzania 2006 , Wema Sepetu amepanga kuzindua filamu yake mpya iitwayo Heaven Sent wiki ijayo na kisha kuoneshwa kwenye majumba ya sinema, Dar es Salaam na kuona moja kwa moja kwenye simu za mkononi kupitia app yake.
Uzinduzi huo amepanga kuufanya katika Ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam, kabla ya kuoneshwa katyika kumbi nyingine.
Kwa mujibu wa dondoo alizowekwa kwenye mtandao wake wa kijamii, nyota huyo amesema kuwa Filamu hiyo iko mbioni kuzinduliwa na kuwaeleza kukaa mkao wa tayari kuisubiri kwani ni nzuri.
Katika filamu hiyo ameingizaq na msanii nyota mwingine wa filamu Tanzania, Gabo Zigamba, huku mwongozaji akiwa ni Neema Ndepanya .
Nyota huyo ameandika katika mtandao wake wa Instagram:
“The Wait Is Over Ladies & Gentlemen… Iam sooo EXCITED…!!! Its Going Down… Ni ileeee Movie inayokuja ku-ShutDown kila Kitu… Tunaanza CountDown kama Hivi…. Nadhani Mnajuaga Sinaga Kazi Mbovu…. I know You all Missed Me…. Well, I missed You too…πππ #RoadToHeaveSentPremier,”
“Kama bado huja download Wema App basi utakuwa unamiss alot… Maana ni kwenye Wema app tutapata nafasi ya kuinunua na kuiangalia huko… Lakini pia pale Mlimani City ndo tutapo enda kuiangalia kwa mara ya kwanza… Yaani Excitement yangu Haielezeki… The Countdown Continues… #RoadToHeaveSentPremier πππ.”
Wema ni mmoja wa wasanii wa bongo movie wanaotesa katika filamu za kibongo akiwa na sifa za kuuvaa uhusika.
Wakati huohuo, Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es Salaam leo imeitaja tena kesi inayomkabili staa huyo ya kukutwa na bangi na na kuitumia na kuiahirisha hadi Septemba 12 na 13, mwaka huu.
Mahakama, chini ya Hakimu Mkazi, Tomeas Simba imesema uamuzi wa kupokea au la kielelezo cha bangi iliyokutwa nyumbani kwa Wema utatolewa Septemba 12.
Wema anakabiliwa na masghitaka ya kukutwa na keti mbili za bangi na msokoto mmoja, pamoja wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa na Matrida.

Comments
Post a Comment