Skip to main content

WANASIMBA WALIVYOPITISHA MABADILIKO YAO


Katika mkutano huo uliofanyika jana na kuhudhuriwa na Waziri wa Afya Jinsia na Watoto, Dk Hamisi Kigwangala, Kaimu Mwenyekiti wa klabu, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema kwamba asilimia 50 ya hisa zitauzwa kwa mwekezaji yeyote au wowote watakaoungana wasiozidi watatu, kwa sharti moja tu la kuwa wanachama wa klabu hiyo.
Abdallah alisema mwekezaji huyo au hao, wanatakiwa kuweka dau lisilopungua Sh. Bilioni 20 ili kupatiwa asilimia 50 ya hisa za klabu, wakati kwa kuanzia wanachama wote wa Simba wamepewa asilimia 10 ya hisa.
Alisema asilimia nyingine 40 zitawekwa kama mtaji wa klabu na zitauzwa kwa wanachama baadaye, lakini wale wawekezaji walionunua asilimia 50 awali, hawataruhusiwa kununua hata hisa moja kwenye asilimia 40 za mtaji.
Na baada ya mkutano wa leo, zoezi litakalofuata ni uhakiki wa wanachama wa klabu hiyo ili kuweza kujua mgawanyo wa asilimia 10 za hisa utakavyokuwa – na itaundwa Kamati maalum ya kupitia maombi ya wawekezaji wanaotaka kununua asilimia 50 ya hisa.
Mgeni rasmi, Dk Kigwangala ameunga mkono mabadiliko hayo na kuwaambia wanachama wa Simba wamechelewa kufanya uamuzi wa mabadiliko hayo, kwani walipaswa kufanya hivyo miaka mingi iliyopita na anaamini klabu nyingine zitafuata nyayo hizo.
“Leo Agosti 20 klabu ya Simba imetengeneza rekodi nyingine baada ya ile ya mwaka 1977 ya kuwafunga Yanga 6-0, na sisi kama Serikali chini ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli tunaunga mkono mabadiliko ya uendeshwaji wa klabu ya Simba,”amesema Dk. Kigwangala.
Kigwangala alisema serikali ya Rais Magufuli inaelewa changamoto za maendeleo ya soka na imekwishaanza kukarabati viwanja vya soka ili kukuza na kuendeleza vipaji na kuviendeleza huku ikijipanga kukusanya kodi.
Alisema rais Magufuli anapenda michezo, amefanikisha hatua za ujenzi wa uwanja wa michezo mkoani Dodoma kwa ufadhili wa Mfalme wa Morocco, Mohammed VI ambao ni zaidi ya Dola za Marekani milioni 100.
Kwa upande wake Mwanasheria aliyefanikisha muundo huo mpya, Evodius Mtawala ambaye ni Katibu Mkuu wa zamani wa klabu hiyo, alisema kwamba baada ya taratibu hizo kukamilika kinachofuata ni Kamati ya Utendaji kutengeneza kamati huru itakayosimamia tenda ambako pia baadaye itatangazwa tenda.
Naye Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Wambura alisema mfumo uliopo katika soka la sasa ni kuendesha mchezo huo kibiashara na kuachana na mfumo wa kisiasa.
Wambura alisema wanachama wakiingia kwenye mfumo wa hisa, wataziingiza familia zao kwenye urithi endelevu hali ambayo ni tofauti na ilivyokuwa awali kwenye uanchama.
“Simba mara nyingi ndio wanakuwa wa kwanza kutekeleza maendeleo na hata ile migogoro ya mara kwa mara haitokuwepo tena na hata makomandoo hawatokuwepo, utakaposababisha Simba ipoteze mapato unajitakia njaa, mpango uliofanikishwa na Simba umeishitua TFF,” alisema Wambura.

Kwa hisani ya blogu ya Bin Zubeiry 

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...