Skip to main content

Walahi Simba wajisikia raha!



Mohammed Ibrahim 'Mo' akipongezwa na wachezaji wenzie baada ya kuifungia Simba bao pekee la ushindi dhidi ya Rayon Sports katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana kwenye maadhimisho ya Siku ya Simba.


Mwandishi wetu

KIWANGO kilichooneshwa na timu ya Simba katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Rayon Sports kimewaacha mashabiki wa timu hiyo wakijisikia raha na kuwa na matumaini makubwa ya kufanya vizuri msimu huu katika mashindano ya ndani na Ligi Kuu ya Vodacom.

Wakicheza mbele ya maelfu ya wanachama, mashabiki na wadau wa soka, waliojitokeza katika maadhimisho ya Tamasha la Simba  katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wacheza ji wa simba walicheza kwa uelewani mkubwa na kuwafanya mashabiki muda mwingi kuwashangilia.

Tamasha hilo majira ya saa 4 asubuhi kwa kufanyika mambo mbalimbali yakiwemo burudani kutoka kwa wasanii kama Snura, Tundaman, Juma Nature na wengine.

Kabla ya mchezo mchezaji Mohammed Hussein Zimbwe alitangazwa kuwa mchezaji bora wa klabu kwa msimu uliopita akichanguliwa na mashabiki wa timu hiyo, huku Abdallah Kibaden akitajwa akipewa tuzo ya heshima  kutokana na  kucheza kwa mafanikio zaidi katika klabu ya Simba.

Kivutio kingine ilikuwa ni pale mshereheshaji alipomtambulisha mlezi wa timu hiyo na mfanyabiashara maarufu Mohamed Dewji 'Mo' ambaye aliandanana na mgeni rasmi katika mchezo huo, January  Makamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira kukagua timu.

Mo pia alizindua app ya Simba ambayo inamwesha mtu mwenye simu ya Smart kufungua na kupata habari mbalimbali kuhusu timu hiyo.


Vifijo na nderemo vilisikika zaidi wakati mshereheshaji, aliposema mchezaji mkongwe wa timu hiyo, Mwinyi kazimoto amekubali kwa hiari yake kuitoa jezi namba nane aliyokuwa akiivaa katika timu hiyo kwa mchezaji mpya  aliyetokea Yanga, Haruna Niyonzima.

Wakati wa mchezo, Emmanuel Okwi, Shiza Kichuya, Mohamed Ibrahim, Kotei walikuwa kivutio kutokana na uelewano mkubwa.

Bao pekee la Simba lilifungwa na  Mohammed Ibrahimu dakika ya
 16 baada ya kupata pasi kutoka kwa Okwi.

Katika kipindi cha pili Niyonzima ambao walikata kiu ya mashabiki wao waliokuwa na hamu ya kuwaona uwanjani.

Niyonzima aliyeingia kipindi cha pili alikiteka 'kijiji cha Simba'  kwa kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo hasa kutokana upigaji wake pasi vyenga vilivyowapa wakati mgumu walinzi wa Rayon na kutengeneza nafasi nzuri ya kufunga, kama John Bocco angekuwa makini angefunga alipobaki yeye na lango la Rayon dakika ya 72.

Bocco angekuwa makini angeweza kufunga mbao hata matatu kutokana na nafasi nzuri alizotengenezewa.

Timu iliyoaanza safu ya ulinzi ya Simba iliyoundwa na kipa Aishi Manula Erasto Nyoni, Jamal Mwambeleko , nahodha Method Mwanjali na Salim Mbonde 'Mndengereko' ilicheza vizuri sana.

Katika kiungo James Kotei, Mohamed Ibrahim 'Mo', Muzamir Yassin walicheza kwa uelewano wakiunganisha mabeki na washambuliaji.

Pamoja na kwamba washambuliaji  Bocco, Shiza Kichuya na Okwi hawakufunga lakini walicheza vizuri.

Shomary  Ally, Junas Mkude, Haruna Niyonzima, Said Ndemla, Laudit Mavugo, Nicholas Gyan na Mwinyi Kazimoto walicheza vizuri na kukonfa nyoyo na mashabiki.

Baada ya mpira kuisha mashabiki wa Simba waliondoka uwanjani wakina na furaha na kusimiliana kila walichokiona uwanjani na kuwa na matumaini timu yao kufanya vizuri katika msimu huu.


Simba: Aishi Manula, Erasto Nyoni, Jamal Mwambeleko/Ally Shomary, Method Mwanjali, Salim Mbonde, James Kotei/Jonas Mkude, Mohamed Ibrahim/Haruna Niyonzima 'Mo', Muzamir Yassin/Said Ndemla, Bocco/Laudit Mavugo, Okwi/Nicholas Gyan na Shiza Kichuya/Mwinyi Kazimoto.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...