Skip to main content

Van Persie akumbukwa Uholanzi


Robin van Persie

AMSTERDAM, Uholanzi
KOCHA wa Uholanzi, Dick Advocaat amemwita tena kwenye kikosi cha timu yake mshambuliaji mkongwe, Robin van Persie kwa ajili ya kuunganika na wenzie kwa ajili ya kujiandaa kwa michezo miwili ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia Urusi mwakani, dhidi ya  Ufaransa na Bulgaria.

Nyota huyo wa Fenerbahce kwa mara ya mwisho aliichezea timu yake ya Taifa Oktoba 2015 ameshaichezea mechi 101. 

Mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal mwenye umri wa miaka 34 ambaye aliwahi pia kuichezea Manchester United ana rekodi ya kufunga mabao mengi kuliko mchezaji yeyote katika timu ya Uholanzi akiweka kimiani mabao 50.

"Bado ninafikiria ni mmoja wa washambuliaji mahiri ambao tunao,'' Advocaat alisema wakati akitangaza kikosi chake na kuongeza anaamini anaweza kutoa mchango muhimu kwa timu ya Uholanzi.

Van Persie ni mmoja kati ya washambuliaji waliojumuishwa katika kikosi sanjari, Memphis Depay wa Lyon na mshambuliaji wa Tottenham, Vincent Janssen.

Baada ya kucheza mechi sita, Uholanzi iko katika nafasi ya tatu kwenye Kundi A,  inazidiwa pointi tatu nyuma na Sweden inayoongoza kundi kwa tofauti ya mabao na Ufaransa. 

Timu zitakazoshinda mechi za mwisho pekee ndizo zitafuzu michuano ya Kombe la Dunia.

Wachezaji wengine wakongwe waliojumuishwa na  kocha huyo kwenye kikosi cha wachezaji 24 pamoja na Van Persie  ni nahodha Arjen Robben na kiungo Wesley Sneijder.

Kikosi kamili kilichoitwa ni:

Makipa: Jasper Cillessen (Barcelona), Maarten Stekelenburg (Everton) na Jeroen Zoet (PSV Eindhoven)
Walinzi: Nathan Ake (Bournemouth), Daley Blind (Manchester United), Wesley Hoedt (Southampton), Matthijs de Ligt (Ajax), Karim Rekik (Hertha Berlin), Kenny Tete (Olympique Lyon), Joel Veltman (Ajax) na  Stefan de Vrij (Lazio).

Viungo: Donny van de Beek (Ajax), Marco van Ginkel (PSV), Tonny Vilhena (Feyenoord), Davy Proepper (Brighton & Hove Albion), Wesley Sneijder (Nice), Kevin Strootman (Roma) na Georginio Wijnaldum (Liverpool).

Washambuliaji: Memphis Depay (Olympique Lyon), Bas Dost (Sporting Lisbon), Vincent Janssen (Tottenham Hotspur), Robin van Persie (Fenerbahce), Quincy Promes (Spartak Moscow) na Arjen Robben (Bayern Munich).

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...