Mwandishi wetu
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limelikumbusha klabu 16 zitakazoshiriki Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza na la Pili kukamilisha usajili kwa mfumo wa Mtanda, TMS kabla ya siku ya mwisho.
Kwa mujibu taarifa ya TFF iliyotolewa na Ofisa habari wake, Alfred Lucas imezikumbusha kalabu kuwa zimebaki siku nne kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili kwa msimu wa 2017/18.
Alisema dirisha la usajili linafungwa Agosti 6, mwaka huu na (TFF), inatoa angalizo kwamba hakuna klabu itakayoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kama haitapata leseni ya klabu.
Amesema baadhi ya klabu hazijachukua fomu za leseni huku pia zilizochukua baadhi hazijarejesha na zilizorejesha zipo ambazo hazikujaza kwa usahihi.
Amesema Klabu ambayo haitapata leseni kutoka TFF, haitakuwa na nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kwa msimu wa 2017/18.
Vigezo sita (6) vya mchezaji kupata leseni ambavyo ni: -
1. Kujazwa fomu ua utimamu wa afya (Medical Form).
2. Bima ya matibabu kwa mchezaji.
3. Barua ya uhamisho (Release Letter).
4. Hati ya Uhamisho wa Kimataifa kwa wachezaji wa kigeni.
5. Mikataba ya wachezaji iliyosajiliwa kwenye mfumo wa usajili TMS
6. Ada ya wachezaji wa kigeni ambayo ni Sh 2,000,000 badala ya dola 2,000 za Marekani.
Mdhamini Mkuu wa michuano hiyo yenye ushindani mkali. Vodacom wanafanya hivyo kwa mujibu wa mkataba wa udhamini.
Katika hatua nyingine, Lucas amesema kesho Alhamisi, Agosti 3, mwaka huu Kampuni ya Vodacom, itatoa vifaa vya mchezo kwa timu zote 16 za Ligi Kuu ya Vodacom.

Comments
Post a Comment