![]() |
| Mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya |
NYON, Uswisi
RATIBA ya Ligi ya Mabingwa imepangwa, mabingwa watetezi, Real Madrid ya Hispania watavaana na Tottenham Hot Spur ya Uingereza katika hatua ya makundi.Spurs imepangwa katika Kundi H na timu nyingine za Borussia Dortmund ya Ujerumani na Apoel ya Cyprus.
Mabingwa wa Scotiland Celtic wako katika kundi B linaloonekana kuwa gumu sanjari na timu za Bayern Munich, Paris St-Germain na Anderlecht.
Mabingwa wa Ligi Kuu England, Chelsea iko pamoja na Atletico Madrid, Roma na Qarabag katika Kundi C, na Mabingwa wa Ligi ya Europa, Manchester United watakutana na Benfica, Basel na CSKA Moscow kwenye Kundi A.
Manchester City, iliyomaliza katika nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu iko Kundi F pamoja na Shakhtar Donetsk, Napoli na Feyenoord, huku Liverpool, iliyoitoa katika hatu ya mchujo Hoffenheimimepangwa pamoja na Monaco, Spartak Moscow, Sevilla na Maribor katika Kundi E.Hatua ya makundi ataanza kupigwa Septemba 12-13, mwaka huu.
Hii ni mara ya kwanza kwa England kuwa na timu tano katika Ligi ya Mabingwa.
Mara ya mwisho Uingereza kuwa na timu sita katika hatu ya makundi ilikuwamsimu wa 2007-08, England ilikuwa na timu za Manchester United, Chelsea, Liverpool na Arsenal na ziliungana na timu mbili za Scotiland za Celtic na Rangers.
United iliyokuwa ikinolewa na Sir Alex Ferguson ilitinga fainali na kuitoa Chelsea iliyokuwa ikinolewa na Avram Grant kwa mikwaju ya penalti.
Makundi Ligi ya MabingwaKundi A: Benfica, Manchester United, Basel, CSKA MoscowKundi B: Bayern Munich, Paris St-Germain, Anderlecht, CelticKundi C: Chelsea, Atletico Madrid, Roma, QarabagKundi D: Juventus, Barcelona, Olympiakos, SportingKundi E: Spartak Moscow, Sevilla, Liverpool, MariborKundi F: Shakhtar Donetsk, Manchester City, Napoli, FeyenoordKundi G: Monaco, Porto, Besiktas, RB LeipzigKundi H: Real Madrid, Borussia Dortmund, Tottenham, Apoel

Comments
Post a Comment