![]() |
| Sol Campbell akiwa na kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu England enzi zake. |
KAMPUNI ya Michezo ya Kubahatisha, SportPesa Timu ya Everton inayoshitiki Ligi Kuu Englangi ikiwa na Wayne Rooney ambaye ni nahodha wa timu ya England leo wanamshusha aliyekuwa beki kisiki wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell.
Campbell, kwa mujibu wa ratiba ya waandaaji wa ziara yake SportPesa, kesho Jumapili kuanzia majira ya saa nane mchana atakuwa katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es salaam kuangalia mechi kati ya timu yake ya zamani ya Asernal na Chelsea ya kuwania Ngao ya Jamii .
Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa, Abbas Tarimba, akiwa nchini Campbell pia atafanya mafunzo kwa timu ya Magnet Uwanja wa Gymkhana na kutembelea timu ya Muungano kwenye Uwanja Karume ambako ataanzia ziara yake.
Tarimba alisema SportPesa inaendelea kuwapa hamasa ya soka Watanzania kwa ujio wa nyota huyo ukiachana na udhamini iliyoutoa kwa Simba, Yanga na Singida United.

Comments
Post a Comment