Haruna Niyonzima
Mwandishi wetu
HATIMAYE klabu ya Simba kiungo mchezeshaji raia wa Rwanda, Haruna Niyonzima akitokea kwa mahasimu wao Yanga aliyoitumikia kwa miaka sita.
Ofisa Habari wa Simba, Haji Sunday Manara akizungumza na waandishi wa habari leo amesema Niyonzima amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu yao, atajiunga na wenzake watakaporudi kwenye kambi yao Afrika Kusini .
“Napenda kuwaambia mashabiki na wapenzi wa klabu ya Simba kwamba, Niyonzima tayari ni mali ya Simba na atawasili hapa nchini wikiendi hii kujiunga na wenzake pamoja na kutembelea maeneo mbalimbali kwenye wiki ya Simba kabla ya Simba Day,” amesema Manara.
Katika hatua nyingine, Simba imezindua rasmi wiki yake ijulikanayo Wiki ya Simba kuelekea kilele cha maadhimisho ya Simba Day Agosti 8, mwaka huu.
Wiki ya Simba inakwenda sanjari na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kutembelea watoto yatima, watoto wanaofanyiwa upasuaji wa moyo na nyingine.

Comments
Post a Comment