Skip to main content

Sharapova ashinda Tenisi Marekani

Maria Sharapova akifurahi baada ya kumshinda Simona Halep.


NEW YORK, Marekani
MARIA Sharapova amerejea kwa kishindo katika mashindano ya tenisi makubwa ya kila mwaka (Grand Slam) kwa kumtoa mchezaji namba mbili kwa ubora duniani, Simona Halep katika michuano ya Marekani.

Mchezaji huyo raia wa Urusi  alishinda seti  2-1 akipata alama 6-4 4-6 6-3 katika pambano ambalo lilihudhuriwa na mashabiki 24,000 mjini New York.

Sharapova mwenye umri wa miaka 30, amecheza mechi ya kwanza ya mashindano ya Grand Slam baada ya kutumikia adhabu yake yake ya kufungiwa kwa miezi 15.


Maria Sharapova (kushoto0 akipena mkono na Simona Halep.

Bingwa huyo wa 2006 na mchezaji bora namba moja duniani alilazimika kucheza mapambano ya kujiweka sawa kabla ya kuruhusiwa kucheza mashindano hayo makubwa na sasa yuko katika nafasi ya 146 kwa ubora.

Sharapova alitumia muda wa saa mbili na dakika 44, Sharapova kabla ya kuibuka na ushindi katika pambano hilo, akimshinda Halep licha ya kufanya makosa 64.

Sharapova anasonga mbele na kesho atapambana na Timea Babos wa  Hungary , ambaye katika ubora duniani yuko namba 59.

Katika mchezo mwingine, Venus Williams aliibuka na ushindi dhidi ya Viktoria Kuzmova ambaye ni yuko katika 135 kwa ubora duniani kwea alama 6-3 3-6 6-2.

Naye Caroline Wozniacki alimshinda Mihaela Buzarnescu kwa seti 2-1 akipata alama 6-1 7-5.

Wozniacki atapambana na  Ekaterina Makarova katika mchezo wake unaofuata.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...